Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb06 kur. 3-5
  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza
  • 2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Eneza Habari Njema za Fadhili Zisizostahiliwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Tunathamini Kupokea Fadhili Zisizostahiliwa za Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Mmewekwa Huru kwa Fadhili Zisizostahiliwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Fadhili Zisizostahiliwa za Mungu Usikose Kusudi Lazo!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb06 kur. 3-5

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

“NA MUWE na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.” Hivyo ndivyo Paulo alivyowasalimu akina ndugu katika barua nyingi ambazo aliyaandikia makutaniko. Maneno hayo yanaonyesha vizuri yale tunayowatakia ninyi nyote.—Efe. 1:2.

Tunathamini sana fadhili zisizostahiliwa ambazo Yehova ametuonyesha kupitia dhabihu ya fidia ya Kristo Yesu. Fidia hiyo imetuwezesha kupata kibali cha Yehova. Hatuwezi kamwe kupata kibali cha Yehova kwa kujifunza Biblia, kuhubiri habari njema, na kufanya mema tu. Msamaha wa dhambi na uzima wa milele si mshahara tunaolipwa kwa jitihada zetu, bali ni zawadi zinazoonyesha fadhili zisizostahiliwa za Yehova kupitia Yesu Kristo.—Rom. 11:6.

Paulo aliwaandikia waamini wenzake hivi: “Tunawasihi ninyi . . . msipokee fadhili zisizostahiliwa za Mungu kisha mkose kusudi lake. Kwa maana anasema: ‘Katika wakati unaokubalika nilikusikia, na katika siku ya wokovu nilikusaidia.’ Tazama! Sasa ndio wakati unaokubalika hasa. Tazama! Sasa ndiyo siku ya wokovu.” Kulikuwa na “wakati unaokubalika” kabla ya kuharibiwa kwa Yerusalemu katika karne ya kwanza. Watu wenye mioyo minyoofu waliompenda Yehova waliokoka kiroho, yaani, walipata kibali chake. Hatimaye waaminifu wote waliokimbia Yerusalemu kabla ya uharibifu wa mwaka wa 70 W.K., waliokoka pia kimwili.—2 Kor. 6:1, 2.

Leo pia, tunaishi katika “wakati unaokubalika” na katika “siku ya wokovu.” Wale ambao Yehova anawakubali kuwa watumishi wake wanaookoka kiroho, nao wana matarajio ya kuokoka kimwili wakati wa “siku kuu ya Yehova,” ambayo sasa imekaribia sana.—Sef. 1:14.

Kwa sababu siku ya Yehova inakuja, sisi tuna wajibu mzito. Ni lazima tuwaonye watu kuihusu na kuwasaidia wale wenye mioyo minyoofu kunufaika na fadhili zisizostahiliwa za Yehova ili wao pia waokoke. Paulo alitambua kwamba wajibu huo ulikuwa mzito sana. Aliandika hivi: “Kwa kweli, ole wangu mimi ikiwa sitangazi habari njema!” Alionyesha pia maoni yake alipoandika maneno haya: “Mimi nina deni . . . kwa wenye hekima na kwa wasio na akili pia: kwa hiyo nina hamu ya kuitangaza habari njema.”—1 Kor. 9:16; Rom. 1:14, 15.

Yehova atatutoza hesabu tukipuuza ile kazi muhimu ya kuwaonya watu. Tunafahamu maneno haya ambayo Yehova alimwambia nabii Ezekieli: “Mwana wa binadamu, nimekufanya kuwa mlinzi katika nyumba ya Israeli, nawe utasikia maneno kutoka katika kinywa changu nawe lazima utawapa maonyo kutoka kwangu. Mimi ninapomwambia mtu mwovu, ‘Hakika utakufa,’ na wewe usimwonye na kusema ili kumwonya mwovu aiache njia yake ya uovu ili kumhifadhi hai, yeye akiwa ni mwovu, katika kosa lake atakufa, lakini damu yake nitaidai kutoka katika mkono wako mwenyewe.”—Eze. 3:17, 18.

Ni vigumu kushughulika na hali katika siku hizi za mwisho. Si rahisi kushughulikia kwa usawaziko familia, kazi, mambo ya kutaniko, na huduma. Isitoshe, wengi kati yenu wameshuka moyo, au wanapambana na magonjwa, uzee, au hata upinzani. Wengi wenu ‘wamelemewa na mizigo.’ Tungependa mjue kwamba tunaelewa hali yenu kama Yesu alivyoelewa hali ya watu katika siku zake aliposema: “Njooni kwangu, nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawaburudisha ninyi.” (Mt. 11:28) Tunawapongeza kwa moyo wote ninyi nyote ambao mnajitahidi kumtumikia Yehova kwa uaminifu licha ya matatizo makubwa na madogo.

Kwa wastani watu 4,762 hubatizwa kila juma, kwa sababu ya bidii yenu ya kuhubiri na kufundisha, na pia kwa sababu ya baraka za Yehova. Makutaniko mapya 1,375 yalianzishwa mwaka wa utumishi uliopita. Tunatarajia kwamba kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa?, ambacho tayari kinapatikana katika lugha zaidi ya 120, kitawasaidia mamilioni ya watu kunufaika kutokana na amani na fadhili zisizostahiliwa za Yehova katika ‘siku hii ya wokovu.’

Mwe na hakika kwamba ndugu wa Baraza Linaloongoza wanawapenda na kusali kwa ajili yenu. Tunawashukuru pia kwa sala zenu kwa ajili yetu.

Ndugu zenu,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki