Andiko la Mwaka wa 2011
‘Pata Kimbilio Katika Jina la Yehova.’—SEFANIA 3:12.
“Uumbaji wote unaendelea kuugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja mpaka sasa.” (Rom. 8:22) Maneno hayo yaliyoongozwa na roho ya Mungu ni ya hakika kabisa. Mamilioni ya watu wamekabili ukosefu wa haki, ukandamizaji, misiba ya asili, magonjwa, umaskini, vita, na uhalifu. Hata sisi tunaomtumikia Yehova tunapatwa na matatizo hayo pia. Zaidi ya hayo, tunadharauliwa, tunachukiwa, na kuteswa kama vile Yesu alivyotendewa.
Ingawa tunakabili matatizo katika ulimwengu huu wa Shetani, hatuvunjiki moyo. Badala yake, tunashangilia kujua kwamba hivi karibuni Yehova atakomesha matatizo yote ulimwenguni. Tumaini letu na imani yetu ni katika Mungu. Ndiyo, tunapata kimbilio katika Yehova, ambaye hawakatishi tamaa hata kidogo waaminifu wake.