Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb15 uku. 166-uku. 167 fu. 3
  • Kiziwi wa Kwanza Kukubali Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kiziwi wa Kwanza Kukubali Kweli
  • 2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Yehova Ameufanya Uso Wake Ung’ae Kuwaelekea’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Uwe Macho Kutafuta Viziwi Katika Eneo Lenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Yehova Alithawabisha Kazi ya Mikono Yangu
    Masimulizi ya Maisha ya Mashahidi wa Yehova
  • Jinsi Mungu Anavyowajali Viziwi
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb15 uku. 166-uku. 167 fu. 3

JAMHURI YA DOMINIKA

Kiziwi wa Kwanza Kukubali Kweli

José Pérez

  • ALIZALIWA 1960

  • ALIBATIZWA 1982

  • HISTORIA FUPI Alipokuwa mvulana, José alivutwa kwenye kweli kwa sababu ya upendo alioonyeshwa kutanikoni, hata ingawa ndugu na dada hawakujua lugha ya ishara.

Picha katika ukurasa wa 166

NILIPOKUWA mtoto, nilipoteza uwezo wa kusikia na kulazimika kujifunza lugha ya ishara katika shule ya viziwi. Nilipata kweli nilipokuwa na umri wa miaka 11, familia fulani ya Mashahidi iliponialika kwenye mikutano ya kutaniko. Nilikaribishwa kwa uchangamfu sana, hata ingawa sikuelewa yaliyofundishwa, niliamua kuendelea kuhudhuria mikutano. Ndugu na dada kutanikoni walinialika kwenye milo na shughuli nyingine mbalimbali.

Nilianza kuhubiri mwaka wa 1982, na nikabatizwa mwaka huohuo. Mwaka wa 1984 nilimwoa Eva, ambaye ni kiziwi pia. Ingawa hatukuelewa kwa kina baadhi ya kweli za Biblia, upendo tulioonyeshwa ulitudhihirishia kwamba hili ni tengenezo la Yehova na tulifurahia kuwa kutanikoni.—Yoh. 13:35.

Mwaka wa 1992, mipango ilifanywa ya kuwafundisha baadhi ya ndugu na dada Lugha ya Ishara ya Marekani (ASL). Baada ya muda, wahubiri hao walianza kuwatafuta viziwi na kuwahubiria habari njema. Kisha, mwaka wa 1994, kazi ya kuwahubiria viziwi iliimarishwa zaidi baada ya wenzi wa ndoa kutoka Puerto Riko kualikwa katika ofisi ya tawi ili kuwafundisha lugha ya ishara ndugu na dada 25.

Baadaye mwaka huo, mimi na Eva tulianza kuhudhuria mikutano katika kikundi hicho kipya cha lugha ya ishara. Tulianza kuelewa kwa kina mafundisho ya Biblia baada tu ya kuhudhuria mikutano iliyofanywa kwa lugha ya ishara, kama vile upinzani wa Shetani dhidi ya enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu mzima na jukumu la Ufalme wa Kimasihi katika kutimiza kusudi la Mungu.

Desemba 1, 1995, makutaniko ya Lugha ya Ishara ya Marekani yalianzishwa jijini Santo Domingo na Santiago. Kufikia Agosti 2014, kulikuwa na makutaniko 26 na vikundi 18 vya lugha ya ishara.

Mimi na Eva tuliwafundisha watoto wetu watatu lugha ya ishara kuwa lugha yao ya asili. Mwana wetu mkubwa, Éber, anasaidia kutafsiri lugha ya ishara katika ofisi ya tawi ya Marekani. Ninatumikia nikiwa mtumishi wa huduma kutanikoni, na Eva ni painia wa kawaida.

Ongezeko la kazi ya kuhubiri katika Lugha ya Ishara ya Marekani tangu 1995 mpaka 2014

  • 1995

    Makutaniko 2

    Picha katika ukurasa wa 167
  • 2014

    Makutaniko 26 na vikundi 18

    Picha katika ukurasa wa 167
    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki