Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb17 kur. 128-129
  • Mume Wangu Hakuweza Kuacha Kusoma!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mume Wangu Hakuweza Kuacha Kusoma!
  • 2017 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Georgia—Urithi wa Kale Uliohifadhiwa
    Amkeni!—1998
  • Kunufaika kwa Usomaji wa Biblia Kila Siku
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Wanapoisoma na Wanavyonufaika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Jinsi Unavyoweza Kunufaika Zaidi Unaposoma Biblia
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
2017 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb17 kur. 128-129

GEORGIA

Mume Wangu Hakuweza Kuacha Kusoma!

Marina Kopaliani

  • ALIZALIWA 1957

  • ALIBATIZWA 1990

  • HISTORIA FUPI Marina na mume wake, Badri, walikuwa wahubiri wenye bidii huku wakiwalea wana wao wawili. Baadaye, Badri alitumikia katika Halmashauri ya Nchi na alibaki mwaminifu hadi alipokufa mwaka 2010.

Marina Kopaliani

Mwaka 1989, mimi na mume wangu tulikutana na Mashahidi katika nyumba ya jirani yetu. Ndugu Givi Barnadze, aliyekuwa akijifunza Biblia na jirani zetu, hakuwa na Biblia kwa sababu ilikuwa vigumu kupata Biblia nchini Georgia wakati huo.

Tulithamini tuliyosikia na tukatamani kupata Biblia. Mume wangu alipokutana na kaka yake, alimwambia kwamba anatafuta Biblia. Kwa kushangaza, kaka yake alimjibu kwamba alikuwa amenunua Biblia ya Kigeorgia muda mfupi tu uliopita na angefurahi kumpa Biblia hiyo ikiwa zawadi.

Badri aliporudi nyumbani, aliketi mezani na kusoma Biblia hiyo hadi usiku ulipoingia. Siku iliyofuata, aliamka na kuendelea kusoma. Niliporudi kutoka kazini siku hiyo, nilimkuta ameketi mezani, akiendelea kusoma Maandiko. Hakuweza kuacha kusoma! Kwa hiyo, nilimpendekezea achukue likizo ya siku chache ili amalize kusoma. Kwa muda mfupi, alimaliza kusoma Biblia nzima.

Baadaye, tulipoanza kusoma kitabu Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele na Ndugu Barnadze, tulifurahi sana kuwa na Biblia yetu. Mambo yalienda vizuri kwa sababu hatukuwa na nakala zetu za kitabu cha Kweli na mwalimu wetu hakuwa na Biblia! Mwaka mmoja hivi baadaye, mimi na Badri tulibatizwa.

Marina and Badri Kopaliani
    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki