Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb17 kur. 136-137
  • Niliona kwa Macho Yangu Mwenyewe Kile Ambacho Biblia Inasema!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Niliona kwa Macho Yangu Mwenyewe Kile Ambacho Biblia Inasema!
  • 2017 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • “Yehova, Umenipata!”
    Amkeni!—2004
  • Nilihisi Nimefanikiwa Maishani
    2017 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Sababu kwa Nini Watu wa Namna Zote Wanakuwa Mashahidi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Maswali Matatu Yalibadili Maisha Yangu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
2017 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb17 kur. 136-137

GEORGIA

Niliona kwa Macho Yangu Mwenyewe Kile Ambacho Biblia Inasema!

Pepo Devidze

  • ALIZALIWA 1976

  • ALIBATIZWA 1993

  • HISTORIA FUPI Alilelewa katika Kanisa Othodoksi la Georgia na alishikamana sana na desturi zake. Baada ya kujifunza kweli ya Biblia, alitumikia Betheli pamoja na mume wake. Sasa wanatumikia wakiwa mapainia wa pekee.

Pepo Devidze

NILISIKIA kuhusu Mashahidi kwa mara ya kwanza nilipokuwa mwanafunzi wa chuo jijini Kutaisi. Jirani yangu aliniambia kwamba Mashahidi hawatumii sanamu katika ibada yao na hawaamini kwamba Yesu ni Mungu Mweza-Yote. Mambo hayo yalipingana na mambo niliyoamini na kuyapenda nikiwa Mkristo Mwothodoksi.

Niliporudi katika mji wa nyumbani wa Tsageri, katika kiangazi cha mwaka 1992, niligundua kwamba Mashahidi wa Yehova walikuwa huko pia. Mama yangu alikuwa amesikia mambo mengi mazuri kuhusu Mashahidi wa Yehova. Kwa sababu bado nilikuwa na maoni yasiyofaa kuwahusu, aliniambia, “Nenda ujionee mwenyewe mambo wanayofundisha.”

Mapainia wawili, Ndugu Pavle na Ndugu Paata, walitembelea kwa ukawaida familia moja katika ujirani wetu. Majirani wengi walichukua nafasi hiyo kuwasikiliza na kuwauliza maswali. Kwa hiyo, niliamua kuhudhuria mazungumzo hayo. Kila mara nilipouliza swali, ndugu hao walifungua Biblia na kuniomba nisome. Jambo hilo lilinigusa moyo sana, kwa kuwa niliona kwa macho yangu mwenyewe kile ambacho Biblia inasema!

Muda mfupi baadaye, nilijiunga na kikundi ambacho kilikuwa kikijifunza Biblia na ndugu hao. Katika majira ya kiangazi mwaka uliofuata, kumi kati yetu tulibatizwa. Baadaye, mama yangu pia akawa Shahidi wa Yehova.

Ninapokumbuka pindi hizo, ninashukuru sana kwamba ndugu hao walijibu maswali yangu yote kwa kuniruhusu nisome majibu kwenye Biblia. Hilo lilinisaidia kufikia mkataa unaofaa mambo niliyoamini yalipokosolewa. Ninapokumbuka jinsi kusoma majibu kwenye Biblia kulivyonisaidia, ninatumia njia hiyohiyo kuwasaidia wengine wathamini kweli.

Pepo Devidze akiwa na mume wake
    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki