Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb17 kur. 6-10
  • Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita
  • 2017 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Makao Makuu na Ofisi ya Tawi Yahamishwa
  • Maendeleo ya Ujenzi Huko Warwick
    2016 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Tengenezo Lililo Mwendoni
    2014 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
  • Maendeleo ya Haraka Huko Warwick
    2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Walijitoa Wenyewe kwa Hiari​—New York
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
2017 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb17 kur. 6-10
Mwingilio na eneo la mnara wa makao makuu ya ulimwenguni kote huko Warwick, NY

Warwick, NY: Makao Makuu ya Ulimwenguni Pote

Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita

ULIMWENGU wa Shetani unapoendelea kupata pigo moja baada ya lingine, Waabudu wa kweli wa Yehova wanaendelea kuwa na “mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.” (1  Kor. 15:58) Ripoti ifuatayo inaonyesha jinsi ambavyo Mashahidi wa Yehova duniani kote wameazimia ‘kumtegemea Yehova . . . , kufanya mema . . . , na kutenda kwa uaminifu.’—Zab. 37:3.

Makao Makuu na Ofisi ya Tawi Yahamishwa

Upanuzi wa majengo yaliyoko Wallkill nchini Marekani, ulikamilika Februari 1, 2016, na hivyo kuruhusu Halmashauri ya Tawi ya Marekani, Idara ya Utumishi, na idara nyingine za tawi la Marekani kuhamia huko. Pia, kwa kuwa kazi ya ujenzi wa makao makuu mapya yaliyopo Warwick inakaribia kukamilika, familia ya Betheli ya Brooklyn imekuwa na kazi kubwa sana ya kuhama kutoka Jijini New York na kwenda maeneo ya pembezoni.

Ramani inayoonyesha majengo na mazingira ya Betheli huko Marekani; makao ya Wallkill; mnara na eneo zima la Warwick

Jumatatu, Aprili 3, 2017, makao makuu ya ulimwenguni pote ya Warwick yatakuwa wazi kwa ajili ya kutembelewa, ambapo kutakuwa na sehemu tatu za matembezi ya kibinafsi na matembezi yanayoongozwa na mtu aliyeteuliwa.

  1. “Biblia na Jina la Mungu” ni sehemu inayoonyesha Biblia ambazo hazipatikani kwa sasa, na vilevile mambo yanayothibitisha kwamba jina la Mungu linapatikana kwenye Maandiko.

  2. “Watu kwa Ajili ya Jina la Yehova” ni sehemu yenye picha zinazoonyesha historia ya kiroho ya Mashahidi wa Yehova, ikionyesha jinsi ambavyo Yehova amewaongoza, kuwafundisha, na kuwapanga watu wake ili kufanya mapenzi yake.

  3. “Makao Makuu ya Ulimwenguni—Imani Yenye Matendo” ni sehemu inayoonyesha jinsi halmashauri za Baraza Linaloongoza zinavyowasaidia watu wa Yehova kukutanika, kufanya wanafunzi, kupata chakula cha kiroho, na kuonyeshana upendo miongoni mwao.

Wageni watakuwa huru kufanya matembezi ya kibinafsi siku za Jumatatu hadi Ijumaa, kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni. Pia, wageni watatembezwa kwa dakika 20 kwenye baadhi ya sehemu katika Jengo la Ofisi na maeneo mbalimbali ya Betheli. Fursa hiyo ya kutembezwa kifupi itapatikana siku za Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 5:00 asubuhi na kuanzia saa 7:00 alasiri hadi saa 10:00 jioni.

Kabla ya kupanga kutembelea, tafadhali tazama jw.org/sw na utafute kwenye KUTUHUSU > OFISI NA MATEMBEZI > Marekani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki