Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 189
  • Je, Ninaweza Kupata Faraja Katika Biblia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Ninaweza Kupata Faraja Katika Biblia?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Matatizo
  • Kifo cha mpendwa
  • Kuhisi hatia kupita kiasi
  • Huzuni
  • Ugonjwa
  • Mkazo na mahangaiko
  • Vita
  • Wasiwasi kuhusu wakati ujao
  • Biblia Inasema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Jinsi Biblia Inavyoweza Kuwasaidia Wanaume Kukabiliana na Mahangaiko
    Habari Zaidi
  • Ninahisi Nina Hatia​—Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Nijihisi Vizuri?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Mtupie Yehova Mahangaiko Yako Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 189
Mwanamke akitabasamu kwa sababu ya kusoma Biblia.

Je, Ninaweza Kupata Faraja Katika Biblia?

Jibu la Biblia

Ndiyo. (Waroma 15:4) Chunguza mistari ya Biblia ambayo imewafariji watu wengi wanaokabiliana na hali ngumu na kushuka moyo.

Katika makala hii

  • Matatizo

  • Kifo cha mpendwa

  • Kuhisi hatia kupita kiasi

  • Huzuni

  • Ugonjwa

  • Mkazo na mahangaiko

  • Vita

  • Wasiwasi kuhusu wakati ujao

Matatizo

Zaburi 23:4: “Hata nikitembea katika bonde lenye kivuli kizito, siogopi madhara yoyote, kwa maana wewe uko pamoja nami.”

Maana: Unaposali kwa Mungu na kutegemea mwongozo wa Neno lake, Biblia, unaweza kukabiliana na matatizo kwa ujasiri.

Wafilipi 4:13: “Kwa mambo yote nina nguvu kupitia yule anayenipa nguvu.”

Maana: Mungu anaweza kukupa nguvu za kukabiliana na tatizo lolote.

Ili kujifunza mengi zaidi kuhusu jinsi Biblia inavyoweza kukusaidia kukabiliana na matatizo ya muda mrefu, ona makala “Changamoto: Hali Zisizoweza Kubadilika.”

Kifo cha mpendwa

Mhubiri 9:10: “Hakuna kazi wala mipango wala ujuzi wala hekima Kaburini.”

Maana: Wale ambao wamekufa hawateseki na hawawezi kutudhuru. Hawajui lolote.

Matendo 24:15: “Kutakuwa na ufufuo.”

Maana: Mungu anaweza kuwafufua wapendwa wetu.

Ili kujifunza mengi zaidi kuhusu jinsi Biblia inavyoweza kukusaidia kukabiliana na kifo cha mpendwa, ona makala “Huzuni ya Kufiwa—Jinsi ya Kukabiliana Nayo.”

Kuhisi hatia kupita kiasi

Zaburi 86:5: “Kwa maana wewe, Ee Yehova,a ni mwema na uko tayari kusamehe; una upendo mwingi mshikamanifu kwa wote wanaokuitia.”

Maana: Mungu huwasamehe wale ambao wanajutia makosa yao ya zamani na kuazimia kutoyarudia.

Zaburi 103:12: “Kama mashariki ilivyo mbali sana na magharibi, ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali sana na sisi.”

Maana: Mungu anaposamehe anaweka makosa yetu mbali sana na sisi. Hatukumbushi makosa hayo tena na tena ili kutulaumu au kutuadhibu.

Ili kujifunza mengi zaidi kuhusu jinsi Biblia inavyoweza kukusaidia kukabiliana na hisia za kwamba una hatia kupita kiasi, ona makala, “Ninahisi Nina Hatia—Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Nijihisi Vizuri?”

Huzuni

Zaburi 31:7: “Umeona dhiki yangu; unajua mateso makali yaliyo ndani yangu.”

Maana: Mungu anajua vizuri mateso yote unayokabili. Anaelewa hisia zako za ndani kabisa​—hata wengine wanaposhindwa kukuelewa.

Zaburi 34:18: “Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo; huwaokoa waliopondeka roho.”

Maana: Mungu anaahidi kukutegemeza unapokuwa na huzuni. Anaweza kukupa nguvu za kukabiliana na huzuni.

Ili kujifunza mengi zaidi kuhusu jinsi Biblia inavyoweza kukusaidia kukabiliana na huzuni, tazama video Acha Kuhuzunika, Changamka!

Ugonjwa

Zaburi 41:3: “Yehova atamtegemeza kwenye kitanda chake cha ugonjwa.”

Maana: Mungu anaweza kukusaidia kukabiliana na ugonjwa kwa kukupatia amani ya akili, nguvu, uvumilivu, na hekima ya kufanya maamuzi yenye busara.

Isaya 33:24: “Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’”

Maana: Mungu anaahidi kwamba wakati utafika ambapo wanadamu wote watakuwa na afya njema.

Ili kujifunza mengi zaidi kuhusu jinsi Biblia inavyoweza kukusaidia kukabiliana na ugonjwa, ona makala “Jinsi ya Kukabiliana na Tatizo la Afya.”

Mkazo na mahangaiko

Zaburi 94:19: “Mahangaiko yaliponilemea, ulinifariji na kunibembeleza.”

Maana: Tukimtegemea Mungu wakati ambapo tuna mkazo, atatusaidia tuwe watulivu.

1 Petro 5:7: “[Tupeni] mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.”

Maana: Mungu anatujali tunapoteseka. Anatualika tumwambie matatizo yetu kupitia sala.

Ili kujifunza mengi zaidi kuhusu jinsi Biblia inavyoweza kukusaidia kukabiliana na mkazo na mahangaiko, ona makala, “Jinsi ya Kukabiliana na Mkazo.”

Vita

Zaburi 46:9: “Anakomesha vita katika dunia yote.”

Maana: Hivi karibuni Ufalme wa Mungu utakomesha vita duniani kote.

Zaburi 37:11, 29: “Wapole wataimiliki dunia, nao watafurahia kwelikweli wingi wa amani. . . . Waadilifu wataimiliki dunia, nao wataishi humo milele.”

Maana: Watu wema watafurahia amani duniani milele.

Ili kujifunza mengi zaidi kuhusu kwa nini tunaamini kwamba Ufalme wa Mungu uko karibu, ona makala “Ufalme wa Mungu Utaanza Kutawala Dunia Lini?”

Wasiwasi kuhusu wakati ujao

Yeremia 29:11: “‘Ninajua vizuri mawazo ninayofikiria kuwaelekea ninyi,’ asema Yehova, ‘mawazo ya amani, wala si ya msiba, ili niwape ninyi wakati ujao na tumaini.’”

Maana: Mungu anawahakikishia watu wake kwamba hivi karibuni watafurahia maisha mazuri sana.

Ufunuo 21:4: “Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”

Maana: Mungu anaahidi kukomesha mambo yote mabaya unayoona yakitukia leo.

Ili kujifunza mengi zaidi kuhusu ahadi za Biblia za wakati ujao, ona makala “Tumaini Bora la Wakati Ujao.”

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu. (Zaburi 83:18) Ona makala “Yehova Ni Nani?”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki