Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 97
  • Kwa Nini Niombe Msamaha?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Niombe Msamaha?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa nini uombe msamaha?
  • Jinsi ya kuomba msamaha
  • Vijana wenzako wanasema nini
  • Je, kwa Kweli Wahitaji Kuomba Radhi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Jinsi ya Kuomba Msamaha
    Amkeni!—2015
  • Kwa Nini Ni Vigumu Sana Kuomba Msamaha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kuomba Msamaha—Ni Njia Bora ya Kufanya Amani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 97
Mwanafunzi akikemewa na mwalimu darasani.

VIJANA HUULIZA

Kwa Nini Niombe Msamaha?

Ungefanya nini ikiwa ungekabili hali zifuatazo?

  1. Mwalimu anakukemea kwa sababu ya kusumbua darasani.

    Je, umwombe mwalimu msamaha—hata ikiwa unafikiri amekukemea kupita kiasi?

  2. Rafiki yako anagundua kwamba umesema mambo mabaya kumhusu.

    Je, umwombe msamaha rafiki yako—hata ikiwa unafikiri jambo ulilosema lilikuwa sahihi?

  3. Baba yako anakukasirisha kwa hiyo unazungumza naye kwa njia isiyo na heshima.

    Je, umwombe baba yako msamaha—hata ikiwa unafikiri yeye ndiye aliyekuwa na makosa?

Jibu la maswali yote matatu ni ndiyo. Lakini kwa nini uombe msamaha, hata ikiwa unahisi kwamba ulikuwa na sababu nzuri ya kufanya ulichofanya?

  • Kwa nini uombe msamaha?

  • Jinsi ya kuomba msamaha

  • Vijana wenzako wanasema nini

Kwa nini uombe msamaha?

  • Kuomba msamaha ni ishara ya ukomavu. Unapokubali makosa yako, unaonyesha kwamba unasitawisha sifa muhimu utakazohitaji utakapokuwa mtu mzima.

    “Kuwa na unyenyekevu na subira kunaweza kutusaidia kuomba msamaha na kumsikiliza yule mtu mwingine.”—Rachel.

  • Kuomba msamaha kunakuwezesha kufanya amani. Watu wanaoomba msamaha wanaonyesha kwamba wanahangaikia kufanya amani kuliko kuthibitisha kwamba hawajafanya makosa au kuonyesha yule mtu mwingine ndiye aliyekosea.

    “Hata ikiwa unahisi hujakosea, lengo linapaswa kuwa kufanya amani. Kusema ‘naomba msamaha’ hakugharimu chochote, lakini kunaweza kukusaidia udumishe urafiki wenu.”—Miriam.

  • Kuomba msamaha kunakufanya ujihisi vizuri. Hisia unazopata unapomuumiza mtu mwingine zinaweza kuwa mzigo wenye kulemea. Lakini unapoomba msamaha, mzigo huo unakuondokea.a

    “Kuna nyakati ambazo nilizungumza kwa hasira na baba na mama. Nilijihisi vibaya, lakini ilikuwa vigumu kwangu kuomba msamaha. Hata hivyo, sikuzote nilipoomba msamaha nilijihisi vizuri kwa sababu hilo lilisaidia familia yetu kuwa na amani tena.”—Nia.

    Kijana akiwa amebeba jiwe kubwa mgongoni.

    Hisia unazopata unapomuumiza mtu zinaweza kuwa mzigo wenye kulemea; unapoomba msamaha, mzigo huo unakuondokea

Je, kuomba msamaha kunahitaji jitihada? Ndiyo! Dena, msichana ambaye amehitaji kuomba msamaha mara nyingi kwa sababu ya kumtendea mama yake kwa njia isiyo na heshima, anasema hivi: “Si rahisi kusema, ‘naomba msamaha.’ Unahisi ni kana kwamba kuna kitu kimekwama kooni na maneno hayawezi kutoka!”

Jinsi ya kuomba msamaha

  • Ikiwezekana, omba msamaha uso kwa uso. Kuomba msamaha ukiwa mbele ya yule uliyomkosea kunampa nafasi ya kuona kwamba kwa kweli unasikitishwa na kosa lako. Lakini ukiomba msamaha kupitia ujumbe wa simu, huenda asihisi kwamba ombi lako linatoka moyoni. Hata ujumbe wako ukiambatanishwa na picha ndogo yenye uso wa mtu aliyehuzunika (emoji), huenda usionekane kuwa wa kweli.

    Dokezo: Ikiwa huwezi kuomba msamaha uso kwa uso, jaribu kupiga simu au kuandika ujumbe kwenye kadi. Njia yoyote utakayoamua kutumia, chagua maneno yako vizuri.

    Kanuni ya Biblia: “Moyo wa mwadilifu hutafakari kabla ya kujibu.”—Methali 15:28.

  • Omba msamaha haraka. Ukisubiri muda mrefu bila kuomba msamaha, huenda hali itazidi kuwa mbaya na uhusiano wako na mtu uliyemuumiza utazidi kuzorota.

    Dokezo: Jiwekee lengo—kwa mfano, ‘Leo nitaomba msamaha.’ Amua mapema utaomba msamaha wakati gani kisha ufanye hivyo.

    Kanuni ya Biblia: “Suluhisha mambo upesi.”—Mathayo 5:25.

  • Omba msamaha kutoka moyoni. Kusema tu “samahani basi kama nilikukosea” si kuomba msamaha! Msichana anayeitwa Janelle anasema, “Yule uliyemkosea atakuheshimu ikiwa ataona unakubali kosa lako.”

    Dokezo: Usiweke masharti unapoomba msamaha. Kwa hiyo, usiseme, “Nitaomba msamaha kwa kosa langu ikiwa wewe pia utaomba msamaha.”

    Kanuni ya Biblia: “Tufuatilie mambo yanayoleta amani.”—Waroma 14:19.

Vijana wenzako wanasema nini

Valerie.

“Ninahitaji unyenyekevu mwingi ili kuomba msamaha—hasa ninapohisi kwamba sikukosea kabisa. Lakini hata hali inapokuwa hivyo, mimi hujaribu kuzungumza kwa njia inayofaa na yenye kutia moyo. Lengo langu ni kuzima moto, si kuuchochea.”—Valerie.

Philip.

“Unapokuwa tayari kuomba msamaha, unaonyesha kwamba unapendezwa zaidi na wengine. Huenda ukaaibika kuomba msamaha, lakini hilo litakufanya uwe rafiki mzuri na kuboresha urafiki wenu.”—Philip.

Kendall.

“Nyakati nyingine mambo madogo sana humfanya mtu akasirike kupita kiasi. Lakini hilo halimaanishi kwamba mimi sijakosea na yeye ndiye aliyekosea. Inafaa kufikiria kosa langu limemwathirije. Ikiwa jambo nililosema au kufanya limemuumiza mtu, ninapaswa kuomba msamaha.”—Kendall.

Pitio: Kwa Nini Niombe Msamaha?

  • Kuomba msamaha ni ishara ya ukomavu.

  • Kuomba msamaha kunakuwezesha kufanya amani.

  • Kuomba msamaha kunakufanya ujihisi vizuri.

Jinsi ya kufanya hivyo:

  • Ikiwezekana, omba msamaha uso kwa uso.

  • Omba msamaha haraka.

  • Omba msamaha kutoka moyoni.

a Ikiwa ulipoteza au kuharibu kitu cha mwenzako, ni jambo la hekima kulipa au kurekebisha kitu kilichoharibika.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki