Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 45
  • Urusi Yashambulia Ukrainia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Urusi Yashambulia Ukrainia
  • Habari Zaidi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kulingana na Biblia, matukio kama hayo yana umuhimu gani?
  • Kwa nini unaweza kuwa na tumaini kuhusu wakati ujao?
  • Mfalme wa Kaskazini” Ni Nani Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Dini na Vita Nchini Ukrainia—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
  • ‘Hapana Amani kwa Wabaya’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vita Nchini Ukrainia Vyaingia Mwaka wa Pili—Biblia Inatoa Tumaini Gani?
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 45
Ramani ya Ukrainia na nchi zinazozunguka.

Urusi Yashambulia Ukrainia

Asubuhi mapema Februari 24, 2022, jeshi la Urusi lilianza mashambulizi dhidi ya nchi ya Ukrainia, licha ya jitihada za viongozi wa ulimwengu kuepusha vita hivyo. Shambulizi hilo litaathirije ulimwengu? António Guterres, katibu-mkuu wa Umoja wa Mataifa, alisema hivi siku chache zilizopita: “Hatuwezi kuwazia mateso, uharibifu, na madhara ambayo shambulizi hilo litatokeza barani Ulaya na kwa usalama wa ulimwengu wote.”

Kulingana na Biblia, matukio kama hayo yana umuhimu gani?

  • Yesu Kristo alitabiri wakati ambapo “taifa litapigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme.” (Mathayo 24:7) Ili uone jinsi Biblia inavyoonyesha kwamba vita leo vinatimiza unabii huo wa Yesu, soma makala yenye kichwa “Ni Nini Ishara ya ‘Siku za Mwisho’?”

  • Kitabu cha Biblia cha Ufunuo kinalinganisha vita na mpanda-farasi aliyeketi juu ya “farasi mwenye rangi ya moto” ambaye anakuja “kuondoa amani duniani.” (Ufunuo 6:4) Ili kuona jinsi unabii huo unavyohusiana na vita leo, soma makala yenye kichwa “Wapanda Farasi Wanne—Jinsi Wanavyokuhusu.”

  • Kitabu cha Danieli kilitabiri ushindani kati ya “mfalme wa kaskazini” na “mfalme wa kusini.” (Danieli 11:25-45) Tazama video yenye kichwa Unabii Uliotimizwa—Danieli Sura 11 ili ujifunze kwa nini Urusi na nchi zinazoiunga mkono zinaweza kutambulishwa kuwa mfalme huyo wa kaskazini.a

  • Pia kitabu cha Ufunuo kinafafanua “vita vya siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufunuo 16:14, 16) Hata hivyo, hiyo si vita kati ya mataifa kama tunayoona sasa. Ili kupata habari zaidi kuhusu matukio hayo ya wakati ujao, soma makala yenye kichwa “Vita vya Har-Magedoni Ni Nini?”

Kwa nini unaweza kuwa na tumaini kuhusu wakati ujao?

  • Biblia inasema kwamba Mungu ‘atakomesha vita katika dunia yote.’ (Zaburi 46:9) Ili ujifunze mengi zaidi kuhusu wakati ujao ambao Mungu ameahidi, soma makala yenye kichwa “Tumaini Bora la Wakati Ujao.”

  • Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasali Ufalme wa Mungu uje. (Mathayo 6:9, 10) Ufalme huo ni serikali ya mbinguni ambayo itatimiza mapenzi ya Mungu duniani, na mapenzi ya Mungu yanatia ndani amani ya ulimwenguni pote. Ili ujifunze jinsi Ufalme huo unavyoweza kukusaidia, tazama video yenye kichwa Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Kuna Mashahidi wa Yehova zaidi ya 129,000 nchini Ukrainia. Kama Mashahidi wengine wanaoishi katika nchi nyingine zote, wanamwiga Yesu kwa kuepuka kuunga mkono upande wowote katika mambo ya kisiasa na kukataa kushiriki katika vita. (Yohana 18:36) Ulimwenguni pote, Mashahidi wa Yehova wanaendelea kutangaza “habari njema ya Ufalme” kuwa suluhisho la matatizo ya wanadamu, kutia ndani vita. (Mathayo 24:14) Tunakualika uwasiliane nasi na kujifunza mengi zaidi kuhusu ujumbe wa Biblia unaotupatia tumaini.

a Ili upate habari kamili kuhusu unabii huu, ona makala zifuatazo “‘Mfalme wa Kaskazini’ Katika Wakati wa Mwisho” na “‘Mfalme wa Kaskazini’ Ni Nani Leo?”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki