Left: Olena Yefremkina/stock.adobe.com; center: lunamarina/stock.adobe.com; right: Rido/stock.adobe.com
ENDELEA KUKESHA!
Unaweza Kumtumaini Nani?—Biblia Inasema Nini?
Watu hukata tamaa wakati wale wanaopaswa kuaminika wanapoonyesha hawatumainiki. Watu wengi wameacha kuwatumaini . . .
viongozi wa kisiasa wanaotanguliza masilahi yao wenyewe badala ya kushughulikia mahitaji ya watu.
vyombo vya habari ambavyo havitoi ripoti sahihi na bila upendeleo.
wanasayansi ambao hawatendi mambo yanayowafaidi wengine.
viongozi wa dini ambao wanajihusisha sana katika siasa badala ya kumwakilisha Mungu.
Inafaa kwamba watu wanajihadhari wanamtumaini nani. Biblia inaonya hivi:
“Msiwategemee wakuu wa dunia; hao ni binadamu tu, hawawezi kuokoa.”—Zaburi 146:3, Biblia Habari Njema.
Unayeweza kumwamini
Biblia inatuambia tunaweza kumtumaini nani: Yesu Kristo. Yeye si mwanamume mzuri tu ambaye aliishi karne nyingi zilizopita. Mungu alimweka rasmi Yesu ‘atawale akiwa Mfalme na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.’ (Luka 1:32, 33) Yesu ni Mfalme wa Ufalme wa Mungu, serikali ambayo sasa inatawala mbinguni.—Mathayo 6:10.
Ili ujifunze kwa nini unaweza kumtumaini Yesu, soma makala yenye kichwa “Mfalme wa Ufalme wa Mungu Ni Nani?” na “Ufalme wa Mungu Utatimiza Nini?”