Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 5
  • Je, Kweli Tunaweza Kujua Ni Nani Aliyeandika Biblia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Kweli Tunaweza Kujua Ni Nani Aliyeandika Biblia?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Biblia Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Ni Nani Aliyeitunga Biblia?
    Amkeni!—2007
  • Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Yaliyomo Katika Hicho Kitabu
    Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 5
Waandikaji watatu wa Biblia

Je, Kweli Tunaweza Kujua Ni Nani Aliyeandika Biblia?

Jibu la Biblia

Watu wengi wameambiwa kwamba hatuwezi kuwa na uhakika kuhusu mtu aliyeandika Biblia. Lakini mara nyingi Biblia inaonyesha wazi watu walioiandika. Sehemu fulani zinaanza kwa maneno kama vile “maneno ya Nehemia,” “maono ya Isaya,” na “neno la Yehova lililomjia Yoeli.”—Nehemia 1:1; Isaya 1:1; Yoeli 1:1.

Waandikaji wengi wa Biblia walikubali kwamba waliandika katika jina la Yehova, Mungu wa pekee wa kweli, na kwamba waliongozwa naye. Manabii walioandika Maandiko ya Kiebrania walitangaza hivi zaidi ya mara 300: “Yehova amesema hivi.” (Amosi 1:3; Mika 2:3; Nahumu 1:12) Waandikaji wengine walipokea ujumbe wa Mungu kupitia malaika.—Zekaria 1:7, 9.

Biblia iliandikwa na wanaume 40 hivi kwa kipindi cha miaka 1,600. Wanaume fulani walitumiwa kuandika zaidi ya kitabu kimoja cha Biblia. Kwa kweli, Biblia ni maktaba ndogo yenye vitabu 66. Ina vitabu 39 vya Maandiko ya Kiebrania, ambavyo kwa kawaida huitwa Agano la Kale, na vitabu 27 vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, ambavyo mara nyingi huitwa Agano Jipya.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki