Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 3
  • Nifanye Nini Ikiwa Ninapenda Kutazama Ponografia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nifanye Nini Ikiwa Ninapenda Kutazama Ponografia?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Unachoweza kufanya
  • Kwa Nini Niepuke Ponografia?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
  • Ninaweza kuepukaje Ponografia?
    Amkeni!—2007
  • Ponografia—Je, Ina Madhara?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kwa Nini Ujiepushe na Ponografia?
    Vijana Huuliza
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 3
Mvulana akitazama ponografia kwenye intaneti

Nifanye Nini Ikiwa Ninapenda Kutazama Ponografia?

Unachoweza kufanya

Elewa ponografia ni nini hasa. Ponografia ni kushushia heshima kitu ambacho Mungu aliumba kiheshimike. Kuelewa hilo kuhusu ponografia kutakusaidia ‘uchukie yaliyo mabaya.’—Zaburi 97:10.

Fikiria madhara. Ponografia huwashushia heshima wahusika. Pia inamdhalilisha mwenye kuitazama. Biblia inasema hivi kwa sababu nzuri: “Mtu mwerevu ni yule ambaye ameona msiba na kujificha.”—Methali 22:3.

Azimia. Mwanamume mwaminifu aliyeitwa Ayubu alisema hivi: “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.” (Ayubu 31:1, Neno—Biblia Takatifu) Wewe pia unaweza ‘kufanya maagano’ yafuatayo:

  • Sitatumia Intaneti nikiwa peke yangu.

  • Nitafunga tovuti yoyote inayotokea ghafula na kuonyesha mambo machafu.

  • Nitazungumza na rafiki mkomavu endapo nitatumbukia tena katika tatizo hili.

Mikono iliyosokotwa kwa uzi

Kadiri unavyozidi kutazama ponografia ndivyo inavyokuwa vigumu kuiepuka

Mwombe Mungu akusaidie. Mtunga-zaburi alimsihi Yehova Mungu hivi: “Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa.” (Zaburi 119:37, Neno—Biblia Takatifu) Mungu anataka ufaulu, na ukimwomba akusaidie, anaweza kukupa nguvu za kufanya yaliyo mema!—Wafilipi 4:13.

Zungumza na mtu. Kuchagua mtu unayeweza kumweleza mambo ya siri ni hatua muhimu inayoweza kukusaidia kuvunja mazoea hayo.—Methali 17:17.

Kumbuka hili: Kila wakati unapoepuka ponografia, unakuwa umepiga hatua kubwa sana. Mwambie Yehova Mungu kuhusu ushindi huo, na umshukuru kwa nguvu alizokupa. Unapoepuka ponografia, unafanya moyo wake ushangilie!—Methali 27:11.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki