Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 6
  • Kwa Nini Wazazi Wangu Hawaniachi Nifurahie Maisha?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Wazazi Wangu Hawaniachi Nifurahie Maisha?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa nini sikuzote wazazi wangu husema hapana?
  • Nifanye nini ili wazazi wangu waseme ndiyo?
  • Kwa Nini Kuna Sheria Nyingi Sana?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
  • Kwa Nini Wazazi Wangu Hawaniachi Nijifurahishe?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
  • Mbona Wazazi Wangu Hawaniachi Nijifurahishe?
    Amkeni!—2011
  • Nifanye Nini Wazazi Wangu Wanapogombana?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 6
Kijana akizungumza na wazazi wake. Masanduku yanaonyesha kifaa cha kucheza michezo ya video, vijana wakicheza dansi kwenye sherehe, na ubao wa kuteleza ulio na magurudumu. Wazazi wake wamekunja mikono kifuani na wamekasirika.

VIJANA HUULIZA

Kwa Nini Wazazi Wangu Hawaniachi Nifurahie Maisha?

Rafiki zako wamekualika kwenye sherehe mwisho juma huu. Unawaomba wazazi wako ruhusa ya kwenda, lakini wanajibu kwa uthabiti, “Hapana.” Jibu lao halikushangazi, kwa sababu walikupa jibu hilohilo wakati uliopita.

Katika makala hii

  • Kwa nini sikuzote wazazi wangu husema hapana?

  • Nifanye nini ili wazazi wangu waseme ndiyo?

  • Vijana wenzako wanasema nini

Kwa nini sikuzote wazazi wangu husema hapana?

Ikiwa unaona ni kana kwamba sikuzote wazazi wako wanakataa maombi yako, huenda ukahisi hawataki ufurahie maisha.

Msichana mmoja anayeitwa Marie alihisi hivyo mara ya kwanza alipopata simu ya mkononi. Anasema hivi: “Baba aliniwekea sheria nyingi kuhusu ni programu zipi ningepakua, ningewasiliana na akina nani, na ningezungumza nao hadi muda gani. Hata hivyo, rafiki zangu waliruhusiwa kufanya chochote walichotaka!”

Jambo la kufikiria: Je, baba ya Marie alikuwa akijaribu kumzuia asifurahie maisha kabisa? Huenda ni nini kilichomhangaisha baba yake?

Gari likiwa barabarani. Pembeni ya barabara kuna ishara ya kudhibiti mwendo iliyoandikwa “50.” Picha ndogo inaonyesha gari linasonga kwa mwendo wa kilomita 50 kwa saa.

Sheria ya kudhibiti mwendo barabarani inakunyima uhuru kwa kadiri fulani, lakini pia inakulinda usipatwe na madhara; ni hivyo pia kuhusu sheria ambazo wazazi wanaweka

Jaribu kufanya hivi: Wazia kwamba wewe ni mzazi, na una kijana ambaye amepata simu ya mkononi. Wewe ungekuwa na wasiwasi upi? Wewe ungemwekea sheria zipi ili kumlinda kijana wako? Wewe ungesema nini ikiwa kijana wako angelalamika kwamba hutaki afurahie maisha?

“Sikuzote baba alisema, ‘Jiwazie jinsi ambavyo ungehisi ikiwa wewe ungekuwa mzazi.’ Kufanya hivyo kulinisaidia kuona faida ya sheria alizoweka na pia sababu ya kuziweka. Ikiwa ningekuwa na watoto, ningetarajia wafuate sheria zilezile ambazo baba yangu aliniwekea.”​—Tanya.

Nifanye nini ili wazazi wangu waseme ndiyo?

Kijana akiwa amenuna na kukunja mikono kifuani huku moshi ukimtoka masikion.

Usifanye hivi: Usinune, usilalamike, wala usibishane.

Kijana akiwa amenuna na kukunja mikono kifuani huku moshi ukimtoka masikion.

“Huwezi kutimiza chochote ukilalamika, na kufanya hivyo kunaweza kukuchosha wewe na wazazi wako kihisia. Ukibishana, wazazi wako watahisi kwamba bado hujakomaa na hustahili kupata uhuru zaidi.”​—Richard.

Jaribu kufanya hivi: Jipatie muda wa kutafakari. Chunguza hali hiyo kwa maoni ya wazazi wako. Jiulize, je, tatizo ni kwamba hawakuamini, au je, ni kwamba hawapendi mazingira unayojiingiza au watu utakaokuwa nao? Kwa nini usizungumze nao kuhusu jambo hilo kwa utulivu, ili uelewe maoni yao?

Balbu.

Dokezo: Unapozungumza na wazazi wako, hakikisha una utatuzi kuhusu mambo yanayowatia wasiwasi. Hata ikiwa wazazi wako watasema hapana, wataelewa jinsi unavyofikiri—nawe utaelewa maoni yao.

“Sikuzote wazazi wangu wana nia nzuri ya kuweka sheria. Si eti wanajaribu kunizuia kufurahia maisha; wangependa tu nifurahie kwa njia nzuri ambayo haitaniletea matatizo.”​—Ivy.

Kanuni ya Biblia: “Mtu mpumbavu humwaga hisia zake zote, lakini mwenye hekima huzizuia kwa utulivu.”​—Methali 29:11.

Msichana akituma na kupokea jumbe na akitumia mtandao wa kijamii usiku sana.

Usifanye hivi: Usifanye kwa siri jambo ambalo wazazi walikukataza.

Msichana akituma na kupokea jumbe na akitumia mtandao wa kijamii usiku sana.

“Nilijaribu kukwepa kutii sheria ambazo baba aliweka kuhusiana na matumizi ya simu. Nilijaribu kutafuta njia za kuwatumia rafiki zangu ujumbe usiku sana au kupakua programu ambazo baba hakuniruhusu niwe nazo. Lakini baadaye aligundua tu, naye akaniwekea sheria kali zaidi kwa sababu sasa hakuniamini. Si hekima kukwepa kufuata sheria.”​—Marie.

Jaribu kufanya hivi: Waonyeshe wazazi wako kwamba unaunga mkono sheria walizoweka na hivyo wakuamini zaidi.

Balbu.

Dokezo: Wazazi wako wanapokuuliza maswali ya moja kwa moja (kwa mfano, “Ni nani atakayekuwa kwenye sherehe hiyo?” “Utarudi nyumbani saa ngapi”), wape majibu hususa na ya kweli. Ukiwapa majibu yasiyo ya wazi, hawatakuamini!

“Uwe na subira. Huenda ikachukua muda mrefu kwa wazazi wako kubadili sheria fulani, lakini wakiona unatii sheria walizoweka tayari, huenda wakakupa uhuru zaidi.”​—Melinda.

Kanuni ya Biblia: “Watiini wazazi wenu katika kila jambo.”​—Wakolosai 3:20.

Mvulana akisihi. Masanduku yanaonyesha vijana wengine watatu.

Usifanye hivi: Usijaribu kuwashinikiza wazazi wako, labda kwa kuwaambia mambo ambayo watoto wengine wa umri wako wanaruhusiwa kufanya.

Mvulana akisihi. Masanduku yanaonyesha vijana wengine watatu.

“Kung’ang’ania jambo lako hakutafanya maisha yako yawe rahisi wala hakutakusaidia kupata unachotaka.”​—Natalie.

Jaribu kufanya hivi: Tumia daftari lenye kichwa “Kutafakari Kuhusu Sheria za Nyumbani” ili kukusaidia kuzungumzia jambo hilo pamoja na wazazi wako.

Balbu.

Dokezo: Chagua wakati ambapo wazazi wako wametulia—si wakati waliporudi tu kutoka kazini au wanapokuwa wamekengeushwa na mambo mengine.

“Wazazi wangependa kuona kwamba una uwezo wa kufanya maamuzi mazuri. Kwa hiyo ninapozungumza nao, mimi hujaribu kutumia hoja kuunga mkono mawazo ninayotoa badala ya kutumia hisia. Ninapofanya hivyo, mara nyingi mimi hufanikiwa kuwasadikisha.”​—Joseph.

Kanuni ya Biblia: “Mheshimu baba yako na mama yako.”​—Waefeso 6:2.

Vijana wenzako wanasema nini

  • Isabella.

    “Nimejifunza kwamba ni lazima familia iwe na sheria ili mambo yaende vizuri katika familia hiyo. Na ingawa zinaitwa sheria, kwa kweli ni miongozo ya ulinzi tu. Ikiwa sheria fulani ya familia inaonekana kuwa kali, huenda wazazi wana sababu nzuri za kuhangaishwa na hali fulani.”​—Isabella.

  • Michael.

    “Nafikiri vijana wanaolelewa chini ya sheria wanakuwa watu wazima bora. Lazima tuwekewe mipaka ili tufurahie maisha. Mipaka hiyo hutusaidia kujifunza kuwajibika na kuepuka madhara.”​—Michael.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki