Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 29
  • Je, Ni Sawa Kusali kwa Watakatifu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Ni Sawa Kusali kwa Watakatifu?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Watakatifu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Je, Tunapaswa Kusali kwa Watakatifu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Je, Ni Sawa Kusali kwa “Watakatifu”?
    Amkeni!—2010
  • Watakatifu wa Kweli Wanaweza Kukusaidiaje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 29

Je, Ni Sawa Kusali kwa Watakatifu?

Jibu la Biblia

Hapana. Biblia inaonyesha kwamba tunapaswa kusali kwa Mungu peke yake, kupitia jina la Yesu. Yesu aliwaambia wanafunzi wake: “Hivi ndivyo mnavyopaswa kusali: Baba yetu uliye mbinguni: Jina lako litukuzwe.” (Mathayo 6:9, Biblia Habari Njema) Hakuwahi kuwaagiza wanafunzi wake wasali kwa watakatifu, malaika, au mtu mwingine yeyote isipokuwa kwa Mungu.

Yesu pia aliwaambia wafuasi wake hivi: “Mimi ni njia, na ukweli na uhai. Hakuna awezaye kwenda kwa Baba ila kwa kupitia kwangu.” (Yohana 14:6, BHN) Yesu tu ndiye amepewa mamlaka na Mungu ya kuomba kwa niaba yetu.—Waebrania 7:25.

Vipi nikisali kwa Mungu na kusali pia kwa watakatifu?

Mungu alisema hivi katika mojawapo wa zile Amri Kumi: “Mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu.” (Kutoka 20:5, BHN) Mungu ni “mwenye wivu” katika njia gani? Mungu anataka tuwe washikamanifu au tumwabudu—kutia ndani sala—yeye peke yake.—Isaya 48:11.

Tunamchukiza Mungu tunaposali kwa mtu yeyote yule, iwe watakatifu au malaika. Mtume Yohana alipotaka kumwabudu malaika fulani, malaika huyo alimkataza na kumwambia: “Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako; sote tunamshuhudia Yesu. Mwabudu Mungu!”—Ufunuo 19:10, BHN

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki