Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 34
  • Je, Mungu Atajibu Sala Zangu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Mungu Atajibu Sala Zangu?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Biblia Inasema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Namna ya Kupata Msaada kwa Sala
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 34

Je, Mungu Atajibu Sala Zangu?

Jibu la Biblia

Ndiyo, atajibu. Biblia na pia masimulizi ya watu yanaonyesha kwamba Mungu hujibu sala. Biblia inasema: “[Mungu] atawatimizia wale wanaomwogopa tamaa yao, naye atakisikia kilio chao cha kuomba msaada, naye atawaokoa.” (Zaburi 145:19) Ili Mungu ajibu sala zako inategemea kwa kiasi kikubwa wewe.

Mambo yaliyo muhimu kwa Mungu

  • Tunapaswa kusali kwa Mungu na si kwa Yesu, Maria, watakatifu, malaika, au sanamu. Yehova Mungu peke yake ndiye “msikiaji wa sala.”​—Zaburi 65:2.

  • Tunapaswa kusali kupatana na mapenzi au matakwa ya Mungu yanayopatikana katika Biblia.​—1 Yohana 5:14.

  • Tunapaswa kusali katika jina la Yesu, na hivyo kutambua mamlaka yake. Yesu alisema: “Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu.”—Yohana 14:6.

  • Tunapaswa kusali kwa imani, tukiomba imani zaidi ikiwa tunaihitaji.​— Mathayo 21:22; Luka 17:5.

  • Tunapaswa kuwa wanyenyekevu na wanyofu. Biblia inasema: “Yehova yuko juu, hata hivyo yeye humwona mnyenyekevu.”​—Zaburi 138:6.

  • Tunapaswa kusali bila kuacha. Yesu alisema: “Endeleeni kuomba, nanyi mtapewa.”​—Luka 11:9.

Mambo yasiyo muhimu kwa Mungu

  • Rangi au taifa lako. “Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.”​—Matendo 10:34, 35.

  • Kikao chako unaposali. Unaweza kusali kwa Mungu ukiwa umeketi, umeinama chini, umepiga magoti, au umesimama.​—1 Mambo ya Nyakati 17:16; Nehemia 8:6; Danieli 6:10; Marko 11:25.

  • Iwe unasali kwa sauti au kimyakimya. Mungu hujibu hata sala za kimyakimya ambazo watu wengine hawasikii.​—Nehemia 2:1-6.

  • Iwe mahangaiko yako ni makubwa au madogo. Mungu anakutia moyo ‘umtupie mahangaiko yako yote juu yake, kwa sababu yeye anakujali wewe.’​—1 Petro 5:7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki