Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 39
  • Je, Mkristo Anaweza Kukubali Matibabu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Mkristo Anaweza Kukubali Matibabu?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Uchaguzi Wako wa Matibabu—Je, Ni Muhimu?
    Amkeni!—2001
  • Je, Mashahidi wa Yehova Wanakubali Matibabu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Mbona Wengi Wanapendezwa na Uwasiliani-roho?
    Amkeni!—2000
  • Je, Mashahidi wa Yehova Hukubali Matibabu?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 39

Je, Mkristo Anaweza Kukubali Matibabu?

Jibu la Biblia

Ndiyo. Yesu alionyesha kwamba wafuasi wake wanaweza kutafuta matibabu aliposema kuwa “watu wenye afya hawahitaji tabibu, bali wenye kuugua ndio wanaomhitaji.” (Mathayo 9:12) Ingawa Biblia si kitabu cha kimatibabu, ina kanuni za kuwaongoza wale wanaotaka kumpendeza Mungu.

Maswali unayopaswa kujiuliza

1. Je, ninaelewa matibabu ninayopendekezewa? Biblia inatushauri tutafute habari zinazotegemeka badala ya ‘kuamini kila neno.’—Methali14:15.

2. Je, nitafute ushauri wa madaktari wengine? Kutafuta ‘washauri wengi’ kunaweza kuwa jambo la maana, hasa ikiwa tatizo lako ni kubwa.—Methali 15:22.

3. Je, matibabu hayo yanavunja amri ya Biblia ya ‘kujiepusha na damu?’—Matendo 15:20.

4. Je, matibabu au mbinu za uchunguzi wa kimatibabu zinatia ndani mazoea ya kuwasiliana na pepo? Biblia inashutumu “mazoea ya kuwasiliana na pepo.” (Wagalatia 5:19-21) Ili ujue ikiwa matibabu fulani yanatia ndani mazoea ya kuwasiliana na pepo, fikiria maswali kama haya:

  • Je, daktari anawasiliana na pepo?

  • Je, matibabu yanategemea imani ya kwamba ugonjwa unasababishwa na miungu iliyokasirika au maadui wanaotumia uchawi?

  • Je, dhabihu, nyimbo za kichawi, au desturi nyingine za kuwasiliana na pepo hutumiwa wakati wa kutengeneza au kutumia dawa?

5. Je, ninahangaikia afya yangu kupita kiasi? Biblia inashauri hivi: “Usawaziko wenu na ujulikane kwa watu wote.” (Wafilipi 4:5) Kuwa na usawaziko kutakusaidia ukazie fikira “mambo yaliyo ya maana zaidi,” kama vile mambo ya kiroho.—Wafilipi 1:10; Mathayo 5:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki