Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 49
  • Ibilisi Anaishi Wapi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ibilisi Anaishi Wapi?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Adui wa Uzima wa Milele
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Shetani
    Amkeni!—2013
  • ‘Mpinge Ibilisi’ Kama Yesu Alivyofanya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Watawala Katika Makao ya Roho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 49

Ibilisi Anaishi Wapi?

Jibu la Biblia

Akiwa kiumbe wa roho, Ibilisi huishi katika makao yasiyoonekana. Hata hivyo, si kwenye moto wa mateso ambapo huwatesa watenda maovu, kama inavyoonyeshwa katika picha iliyo kwenye makala hii.

“Vita mbinguni”

Kwa muda fulani, Shetani Ibilisi alikuwa na uhuru wa kutembea huku na kule katika makao yasiyoonekana ya roho, kutia ndani kusimama mbele za Mungu akiwa pamoja na malaika waaminifu. (Ayubu 1:6) Hata hivyo Biblia ilitabiri kwamba kungekuwa na “vita mbinguni” ambavyo vingesababisha Shetani “kutupwa duniani.” (Ufunuo 12:7-9, Habari Njema kwa Watu Wote) Masimulizi ya Biblia na matukio ya ulimwengu yanathibitisha kwamba vita hivyo tayari vilitokea mbinguni. Ibilisi sasa hawezi tena kurudi mbinguni.

Je, hilo linamaanisha kwamba Ibilisi anaishi mahali fulani hususa duniani? Kwa mfano, jiji la kale la Pergamamu lilionwa kuwa “mahali kilipo kiti cha ufalme cha Shetani” na “mahali anapokaa Shetani.” (Ufunuo 2:13) Kwa kweli, huenda maneno hayo yakarejelea jinsi ambavyo ibada ya kishetani ilivyokuwa imejaa katika jiji hilo. Biblia inasema kwamba Ibilisi anatawala “falme zote za dunia inayokaliwa,” kwa hivyo hakai mahali pamoja duniani na hawezi kurudi mbinguni.​—Luka 4:​5, 6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki