Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 58
  • Je, Biblia Inakataza Kufurahia Ngono?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Biblia Inakataza Kufurahia Ngono?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Maoni Yako Juu ya Ngono—Yanafanyiza Tofauti Gani?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je! Ndoa Yako Yaweza Kufanikiwa?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Uaminifu Katika Ndoa Unamaanisha Nini Hasa?
    Amkeni!—2009
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 58

Je, Biblia Inakataza Kufurahia Ngono?

Jibu la Biblia

Biblia inaonyesha kwamba ngono ni zawadi kwa watu waliofunga ndoa, na hivyo haiwakatazi kufurahia ngono. Mungu alimuumba “mwanamume na mwanamke” na kuona kwamba kila kitu alichofanya “kilikuwa chema sana.” (Mwanzo 1:​27, 31) Alipowaunganisha mwanamume na mwanamke wa kwanza katika ndoa, alisema hivi: “watakuwa mwili mmoja.” (Mwanzo 2:​24) Muungano huo ungewawezesha wafurahie ngono na pia ungewafanya wawe na uhusiano wa karibu sana wa kihisia.

Biblia inafafanua furaha ambayo waume hupata katika ndoa inaposema hivi: ‘Shangilia pamoja na mke wa ujana wako .   . Na maziwa yake yakuleweshe nyakati zote. Upendo wake na ukufurahishe sikuzote.’ (Methali 5:​18, 19) Pia, Mungu anataka wanawake wafurahie ngono. Biblia inasema hivi: “Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.”​—1 Wakorintho 7:3, Union Version.

Kanuni zinazohusu kufurahia ngono

Ni watu waliooana tu ambao Mungu anawaruhusu wafanye ngono, kama vile tunavyosoma katika Waebrania 13:4: “Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi, kwa maana Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.” Watu waliooana wanapaswa kuwa waaminifu na wanapaswa kuwajibika sikuzote kwa mmoja na mwenzake. Wanapata furaha nyingi sana, si kwa kujitanguliza wenyewe, bali kwa kufuata kanuni ya Biblia inayosema: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”​—Matendo 20:35.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki