Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 56
  • Je, Ibilisi Anaweza Kuwaongoza Wanadamu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Ibilisi Anaweza Kuwaongoza Wanadamu?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Biblia Inasema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Je! Viko Viumbe Vibaya vya Kiroho?
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Mpinge Shetani, Naye Atakimbia!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Je, Unaamini Kwamba Ibilisi Yuko?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 56

Je, Ibilisi Anaweza Kuwaongoza Wanadamu?

Jibu la Biblia

Ibilisi na roho waovu wamekuwa na uvutano mkubwa kuelekea wanadamu hivi kwamba Biblia inasema hivi kuwahusu: “Yule Mwovu anauongoza ulimwengu mzima.” (1 Yohana 5:​19, New Century Version) Biblia inaonyesha njia anazotumia Ibilisi kushawishi watu.

  • Uwongo. Biblia inawatia moyo Wakristo “kupigana dhidi ya mbinu zenye uovu za Ibilisi.” (Waefeso 6:​11, NCV) Mbinu moja anayotumia ni kudanganya watu waamini kwamba wawakilishi wake ni wahudumu wa Mungu.​—2 Wakorintho 11:13-​15.

  • Kuwasiliana na Pepo. Ibilisi anawaongoza vibaya watu kupitia watu wanaowasiliana na pepo, wanaotafuta ishara za bahati, na wale wanaofanya uaguzi au unajimu. (Kumbukumbu la Torati 18:10-​12) Matumizi mabaya ya dawa za kulevya, kupumbaza akili, na mbinu fulani za kutafakari zinazotia ndani kuacha akili ikiwa bila wazo lolote, mambo yanayoweza kufanya iwe rahisi kwa mtu kuongozwa na roho waovu.​—Luka 11:24-​26.

  • Dini ya uwongo. Dini zinazofundisha uwongo huwafanya watu wasimtii Mungu. (1 Wakorintho10:20) Biblia inaita mafundisho hayo ya uwongo kuwa “mafundisho ya roho waovu.”​—1 Timotheo 4:1.

  • Kuongozwa na roho waovu. Biblia inataja kuhusu roho waovu walioongoza watu. Watu wenye roho waovu walipigwa upofu, kuwa bubu au kujiumiza wenyewe.​—Mathayo 12:22; Marko 5:​2-5.

Jinsi ya kujiepusha na uvutano wa Ibilisi

Huna sababu ya kuhofu sana kwamba utaongozwa na roho waovu kwa kuwa Biblia inaonyesha jinsi unavyoweza kumpinga Ibilisi:

  • Jifunze kutambua njia anazotumia Ibilisi ili ‘usikose kuzijua mbinu zake.’​—2 Wakorintho 2:​11.

  • Jifunze Biblia na utumie ujuzi huo. Kutumia kanuni za Biblia kutakulinda na uvutano wa Ibilisi.​—Waefeso 6:​11-​18.

  • Ondolea mbali kila kitu kinachohusiana na roho waovu. (Matendo 19:19) Vitu hivyo vinatia ndani muziki, vitabu, magazeti, kadi, na sinema zinazochochea kuwasiliana na pepo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki