Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 72
  • Kitabu cha Ufunuo—Kinamaanisha Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitabu cha Ufunuo—Kinamaanisha Nini?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Iweni Wasomaji Wenye Furaha wa Kitabu cha Ufunuo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Ufunuo—Upeo Wao Wenye Furaha!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Ufunuo 21:1—“Mbingu Mpya na Dunia Mpya”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • Vitu Ambavyo Lazima Vitukie Karibuni
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 72
Mwanamume akisoma kitabu cha Ufunuo anapiga picha akilini ya mnyama-mwitu na wapanda farasi wa Apokalipsi

Kitabu cha Ufunuo​—Kinamaanisha Nini?

Jibu la Biblia

Neno A·po·kaʹly·psis (apokalipsi) ni neno la Kigiriki la kitabu cha Ufunuo ambalo linamaanisha “Kufunua” au “Kufichua.” Neno hilo linatusaidia kuelewa maana ya kitabu cha Ufunuo kwamba kinafichua mambo ambayo yalikuwa yamefichwa na kinafunua matukio yatakayotendeka muda mrefu baada ya kuandikwa. Unabii mwingi ulioandikwa katika kitabu cha Ufunuo bado haujatimizwa.

Muhtasari wa kitabu cha Ufunuo

  • Utangulizi.​—Ufunuo 1:​1-9.

  • Ujumbe wa Yesu kwa yale makutaniko saba.​—Ufunuo 1:10–​3:​22.

  • Maono ya Mungu akiwa ameketi kwenye kiti chake cha enzi mbinguni.​—Ufunuo 4:1-​11.

  • Mfululizo wa maono kadhaa, moja baada ya lingine:

    • Mihuri saba.​—Ufunuo 5:1–​8:6.

    • Tarumbeta saba, tatu za mwisho zinapopigwa zinaleta ole tatu.​—Ufunuo 8:7–​14:20.

    • Mabakuli saba, kila moja ya mabakuli hayo yana tauni ambayo inawakilisha hukumu ya Mungu ambayo inaletwa duniani.​—Ufunuo 15:1–​16:21.

    • Maono ya uharibifu wa adui za Mungu.​—Ufunuo 17:1–​20:10.

    • Maono ya Mungu akileta baraka zake mbinguni na duniani.​—Ufunuo 20:11–​22:5.

  • Umalizio.​—Ufunuo 22:​6-​21.

Mambo yanayoweza kutusaidia kuelewa kitabu cha Ufunuo

  1. Kitabu cha Ufunuo kina ujumbe wenye kutia moyo na ujumbe huo hauwaogopeshi wale wanaomtii Mungu. Ingawa watu wengi hulihusianisha neno “apokalipsi” na msiba mkubwa, kitabu cha Ufunuo kinaanza kwa kusema kwamba wale wanaosoma, wanaoelewa na kutenda kupatana na mambo yaliyoandikwa humo watakuwa na furaha wanapofanya hivyo.​—Ufunuo 1:3; 22:7.

  2. Kitabu cha Ufunuo kinatumia “ishara” nyingi au mifano.​—Ufunuo 1:1.

  3. Majina ya cheo au sifa zinazowakilisha watu au vitu vinavyotajwa katika kitabu cha Ufunuo zinapatikana katika sehemu nyingine za Biblia:

    • Yehova​—‘Mungu wa kweli wa mbinguni’ na Muumba wa vitu vyote.​—Kumbukumbu la Torati 4:​39; Zaburi 103:19; Ufunuo 4:​11; 15:3.

    • Yesu Kristo​—“Mwana-Kondoo wa Mungu.”​—Yohana 1:​29; Ufunuo 5:6; 14:1.

    • Shetani Ibilisi​—Adui ya Mungu.​—Mwanzo 3:​14, 15; Yohana 8:​44; Ufunuo 12:9.

    • Babiloni Mkubwa​—kama Babiloni la kale (Babeli) lilivyokuwa, Babiloni Mkubwa ni adui ya Yehova Mungu na watu wake na ni chanzo cha mafundisho ya uwongo yanayofundishwa katika dini leo.​—Mwanzo 11:​2-9; Isaya 13:​1, 11; Ufunuo 17:​4-6; 18:​4, 20.

    • “Bahari”​—wanadamu waovu wanaompinga Mungu.​—Isaya 57:20; Ufunuo 13:1; 21:1.

    • Mambo mbalimbali yanayolingana na maskani ya kale iliyotumiwa kumwabudia Mungu​—kama vile sanduku la agano, bahari ya kioo (beseni ya kuogea), taa, matoleo ya uvumba wenye manukato, na madhabahu ya kutolea dhabihu.​—Kutoka 25:10, 17, 18; 40:24-32; Ufunuo 4:​5, 6; 5:8; 8:3; 11:19.

    • Wanyama-mwitu​—wanafananisha serikali za wanadamu.​—Danieli 7:​1-8, 17-​26; Ufunuo 13:​2, 11; 17:3.

    • Namba zinatumiwa kwa njia ya mfano.​—Ufunuo 1:​20; 8:​13; 13:18; 21:16.

  4. Maono hayo yanahusu “Siku ya Bwana” ambayo ilianza mwaka wa 1914 Mungu alipomweka Yesu rasmi kuwa Mfalme wa Ufalme wake. (Ufunuo 1:​10) Kwa hiyo basi utimizo mkubwa wa unabii wa kitabu cha Ufunuo unahusu wakati wetu.

  5. Ili tukielewe kitabu cha Ufunuo tunahitaji mambo yaleyale yanayohitajika tunaposoma sehemu nyinginezo za Biblia, yaani, hekima kutoka kwa Mungu na mwongozo kutoka kwa wale ambao tayari wanakielewa.​—Matendo 8:​26-​39; Yakobo 1:5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki