Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 90
  • Je, Ni Lazima Mtu Awe Katika Dini Fulani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Ni Lazima Mtu Awe Katika Dini Fulani?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Biblia Inafundisha Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Dini
    Amkeni!—2014
  • Kuzoea Dini Safi Kwa Ajili Ya Kuokolewa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je, Ni Lazima Uwe Mshiriki wa Dini Fulani?
    Amkeni!—2012
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 90
Kikundi cha watu waliokusanyika ili kuabudu

Je, Ni Lazima Mtu Awe Katika Dini Fulani?

Jibu la Biblia

Ndiyo, kwa sababu Mungu anataka watu wakutane kwa ajili ya ibada. Biblia inasema: “Acheni tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukusanyika pamoja sisi wenyewe.”​—Waebrania 10:24, 25.

Yesu alisema kwamba wafuasi wake wangekuwa katika kikundi kilichopangwa alipowaambia hivi: “Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo kati yenu wenyewe.” (Yohana 13:35) Njia kuu ambayo wanafunzi wa Kristo wangeonyesha upendo huo ni kwa kukutana pamoja na waamini wenzao. Wangepangwa katika makutaniko yanayokutana kwa ukawaida kwa ajili ya ibada. (1 Wakorintho 16:19) Kwa ujumla, wangefanyiza undugu wa ulimwenguni pote.​—1 Petro 2:​17.

Mengi yanahitajika kuliko kuwa tu katika dini fulani

Ingawa Biblia inaonyesha kwamba watu wanapaswa kukutana ili kumwabudu Mungu, haifundishi kwamba mtu anaweza kumpendeza Mungu kwa kuwa tu mshiriki wa dini fulani. Ili mtu apate kibali cha Mungu, dini yake inapaswa kuathiri maisha yake ya kila siku. Kwa mfano, Biblia inasema: “Namna ya ibada iliyo safi na isiyotiwa unajisi kwa maoni ya Mungu wetu na Baba ni hii: kuwatunza mayatima na wajane katika dhiki yao, na kuendelea kujitunza bila doa kutokana na ulimwengu.”​—Yakobo 1:27.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki