Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 93
  • Je, Yesu Alifufuliwa Akiwa na Mwili wa Nyama au wa Roho?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Yesu Alifufuliwa Akiwa na Mwili wa Nyama au wa Roho?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Kristo Anarudi Namna Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Kurudi kwa Kristo Kunaonekanaje?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Ufufuo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Tumaini la Ufufuo Lina Nguvu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 93
Yesu aliyefufuliwa, akiwa na alama ya msumari mkononi mwake, anamtokea mtume Tomasi na wanafunzi wengine akiwa na mwili wa kibinadamu

Je, Yesu Alifufuliwa Akiwa na Mwili wa Nyama au wa Roho?

Jibu la Biblia

Biblia inasema kwamba Yesu “aliuawa katika mwili, lakini akafanywa kuwa hai [akafufuliwa] katika roho.”​—1 Petro 3:18; Matendo 13:34; 1 Wakorintho 15:45; 2 Wakorintho 5:16.

Yesu mwenyewe alisema kwamba hangefufuliwa akiwa na mwili wa nyama na damu. Alisema kwamba angetoa ‘mwili wake kwa ajili ya uzima wa ulimwengu,’ yaani, uwe fidia kwa ajili ya wanadamu. (Yohana 6:​51; Mathayo 20:28) Ikiwa angevaa tena mwili wake alipofufuliwa, angekuwa amebatilisha dhabihu ya fidia aliyokuwa ametoa. Lakini hakufanya hivyo kwa kuwa Biblia inasema kwamba alidhabihu mwili wake na damu yake “mara moja kwa wakati wote.”—Waebrania 9:​11, 12.

Ikiwa Yesu alifufuliwa akiwa na mwili wa roho, wanafunzi wake walimwonaje?

  • Viumbe wa roho wanaweza kuvaa mwili wa kibinadamu. Kwa mfano, malaika walifanya hivyo katika nyakati za kale hivi kwamba wakala na kunywa pamoja na wanadamu. (Mwanzo 18:​1-8; 19:​1-3) Hata hivyo, bado walikuwa viumbe wa roho na wangeweza kuondoka ulimwenguni.​—Waamuzi 13:15-​21.

  • Baada ya Yesu kufufuliwa, alichukua umbo la kibinadamu kwa muda, kama malaika walivyokuwa wamefanya hapo awali. Hata hivyo, akiwa kiumbe wa roho, angeweza kuonekana na kutoweka ghafla. (Luka 24:31; Yohana 20:19, 26) Hakuchukua mwili uleule kila mara alipoonekana. Kwa hiyo, hata marafiki wa karibu walimtambua tu kwa mambo aliyosema na kufanya.​—Luka 24:30, 31, 35; Yohana 20:14-​16; 21:​6, 7.

  • Yesu alipomtokea mtume Tomasi, alivaa mwili uliokuwa na majeraha. Alifanya hivyo ili kuimarisha imani ya Tomasi ambaye alikuwa na shaka kwamba Yesu alikuwa amefufuliwa.​—Yohana 20:24-​29.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki