Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 114
  • Je, Kuna “Dhambi Saba Nzito”?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Kuna “Dhambi Saba Nzito”?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Dhambi Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Mungu Aliye “Tayari Kusamehe”
    Mkaribie Yehova
  • Dhambi
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 114
Mwanamume aliyehuzunika

Je, Kuna “Dhambi Saba Nzito”?

Jibu la Biblia

Biblia haitaji kihususa “dhambi saba nzito.” Hata hivyo, inafundisha kwamba kutenda dhambi nzito kutamzuia mtu asipate wokovu. Kwa mfano, Biblia inataja dhambi nzito kama uasherati, ibada ya sanamu, kuwasiliana na pepo, milipuko ya hasira, na ulevi, kuwa ni “matendo ya mwili.” Kisha inasema hivi: “Wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.”​—Wagalatia 5:19-21.a

Je, Biblia haiorodheshi ‘vitu saba ambavyo ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu’?

Ndiyo, inafanya hivyo. Kulingana na Biblia Habari Njema, Methali 6:16 inasema hivi: “Kuna vitu anavyochukia Mwenyezi-Mungu; naam, vitu saba ambavyo ni chukizo kwake.” Hata hivyo, dhambi zinazoorodheshwa baada ya hapo katika Methali 6:17-19 si orodha kamili. Badala yake inafafanua vitengo vya msingi vinavyowakilisha aina zote za makosa, kutia ndani, mawazo, maneno, na matendo.b

Kuna tofauti gani kati ya “dhambi ambayo huleta kifo” na “dhambi ambayo haileti kifo”?

Biblia inaonyesha wazi kwamba dhambi zote huongoza kwenye kifo. Hata hivyo, tunaweza kuokolewa kutokana na dhambi na kifo kupitia dhabihu ya fidia ya Yesu Kristo. (Waroma 5:12; 6:23) Hivyo, “dhambi ambayo huleta kifo” ni ile ambayo haiwezi kufunikwa na fidia ya Kristo. (1 Yohana 5:16) Mtu ambaye hufanya dhambi ya aina hii ameazimia kabisa kufanya dhambi hivi kwamba hawezi kubadili mtazamo au mwenendo wake. Pia Biblia huirejelea kuwa aina ya dhambi ambayo haiwezi kusamehewa.​—Mathayo 12:31; Luka 12:10.

Orodha ya dhambi saba nzito ilitoka wapi?

“Dhambi saba nzito” zilitokana na orodha iliyotungwa katika karne ya nne W.K iliyotaja mambo maovu manane. Orodha hiyo ilitungwa na Evagrius Ponticus, na ilimchochea mtawa John Cassian kuandika vitabu vilivyohusiana na habari hizo. Katika karne ya sita, Papa Gregory wa Kwanza alibadili orodha ya Cassian ya mambo manane maovu zaidi kuwa orodha ya dhambi saba nzito, au dhambi inayostahili kifo katika theolojia ya kanisa Katoliki: kiburi, pupa, tamaa, wivu, ulafi, hasira, na uzembe. Gregory aliona kuwa hizo ni dhambi ambazo hukumu yake ni kifo na kwamba zinachangia kutokea kwa dhambi nyingine nyingi..

a Orodha ya mambo 15 yanayofanyiza dhambi nzito zinazopatikana kwenye Wagalatia 5:19-21 haijakusudiwa kuwa orodha ya dhambi zote, kwa kuwa baada ya orodha hiyo Biblia inaongezea maneno “mambo ya namna hiyo.” Kwa hiyo, msomaji wa Biblia anatiwa moyo atumie utambuzi kufahamu mambo ambayo hayajaorodheshwa lakini ambayo ni kati ya “mambo ya namna hiyo.”

b Methali 6:16 inatumia msemo wa Kiebrania unaokazia namba ya pili kwa kuitofautisha na ya kwanza. Misemo ya aina hiyo inapatikana mara nyingi katika Maandiko.​—Ayubu 5:19; Methali 30:15, 18, 21.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki