Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 7/1 kur. 2-23
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Habari Zinazolingana
  • Ikiwa Mtu wa Ukoo Ametengwa na Ushirika...
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Kuendeleza Maoni Yaliyosawazika Juu ya Waliotengwa na Ushirika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 7/1 kur. 2-23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Je! kuna wakati wo wote ambapo ingefaa kusali kwa ajili ya mtu ambaye ametengwa na kundi la Kikristo?

Katika wakati uliopita ilifikiriwa kwamba sala za namna hiyo hazingefaa. Na kuna sababu nzuri za Kimaandiko za kuweka vizuizi. Walakini shauri la Biblia linalohusu jambo hilo hupendekeza kufikiria hali ya kila mtu mmoja mmoja badala ya kufanya uamuzi wa jumla.

Hasa 1 Yohana 5:16, 17 hutusaidia kupata maoni ya Mungu. Linasema hivi: “Ikiwa mtu ye yote anamwona nduguye akitenda dhambi isiyo ya kufisha, lazima aombe na Mungu atampa uzima kwa ajili ya wale wanaotenda dhambi isiyo ya kufisha. Kuna dhambi ya kufisha. Sisemi kwamba inampasa kusali kwa ajili ya hiyo. Udhalimu wote ni dhambi, na [hata hivyo] kuna dhambi isiyo ya kufisha.”​—The Riverside New Testament.

Kwanza mtume Yohana ataja “dhambi isiyo ya kufisha,” au, kama vile tafsiri ya New World inavyoitafsiri, “dhambi isiyoleta kifo.” Kwa kuwa sisi sote tu watu wasiokamilika na wadhalimu, sisi sote tuna hatia ya dhambi. (Zab. 51:5; Rum. 3:23; 1 Yohana 3:4) Mtu ambaye ametenda dhambi anahitaji kusali apate rehema nyingi ya Mungu. (1 Yohana 1:8-10) Kama vile anavyoonyesha Yohana wengine pia waweza kusali kwa ajili yake.

Kisha, Yohana ataja “dhambi ya kufisha,” au “dhambi inayoleta kifo.” Hiyo ni nini? Ni dhambi asiyoweza mtu kusamehewa; ni “ya kufisha” kwa kuwa inaongoza kwenye “mauti ya pili,” au mauti ya milele. (Ufu. 21:8) Mapema, Yesu alieleza kwamba mtu anaweza kutenda dhambi kufikia hatua ya kutenda dhambi roho takatifu, dhambi ambayo hakuna msamaha. (Mt. 12:31; Luka 12:10) hali moja na hiyo, mtume Paulo alionyesha kwamba ikiwa mtu anayejua kweli ya Mungu anazoea dhambi makusudi, hangeweza tena kutubu na kupata msamaha.​—Ebr. 6:4-6; 10:26, 27.

Yohana atuambia kwamba tusisali kwa ajili ya mtu kama huyo aliyetenda dhambi “ya kufisha.” Hiyo inatukumbusha maneno ya Mungu kuhusu Waisraeli ambao walitenda dhambi sana hivi kwamba Yeye angeruhusu Wababeli wawapeleke uhamishoni. Mungu alimwambia Yeremia hivi: “Basi, wewe usiwaombee watu hawa, wala usiwapazie sauti yako, wala kuwaombea dua, wala usinisihi kwa ajili yao.”​ —Yer. 7:16-20; 14:11, 12.

Mungu, si sisi hapa duniani, huamua kama mtu ametenda roho takatifu dhambi. Hata hivyo, twaweza kuthamini kutokana na maneno ya Yohana yaliyoongozwa kwa roho kwamba haitupasi kusali kwa ajili ya mtu anayetoa ushuhuda wa kwamba anazoea dhambi makusudi. Vilevile, katika 2 Yohana 9-11 Yohana aliandika juu ya watu wanaoeneza maoni yasiyo ya Kikristo. Sala kwa ajili yao ingemchukiza Mungu.

Kwa hiyo, je! inatupasa kuamua kwamba mtu anayetengwa na ushirika kwa sababu ya dhambi ambayo hakutubia inaelekea ametenda dhambi inayoleta kifo,” ambayo haitupasi kuomba kwa ajili ya hiyo? Si lazima iwe hivyo. Kumbuka kwamba katika kundi la karne ya kwanza la Korintho mwanamume fulani aliangukia uasherati. Alikosa kutubu kwa kitambo na kwa hiyo ikawa lazima kumtenga na ushirika. (1 Kor. 5:1, 9-13) Hata hivyo, inaelekea kwamba, baada ya muda fulani kupita alitubu na akarudishwa. (2 Kor. 2:5-10) Hiyo inaonyesha kwamba ijapokuwa alikuwa ametengwa na ushirika, yeye hakuwa ametenda dhambi iletayo kifo, ambayo Wakristo hawapaswi kusali juu yake. Inaweza kuwa vivyo hivyo leo.

Mtu anapotengwa na ushirika, haionekani waziwazi wakati huo kama dhambi hiyo ‘italeta kifo’ au hapana. Walakini baada ya wakati fulani kupita ushuhuda wa kutubu na kugeuka huenda ukaanza kuonekana. (Linganisha Matendo 2:36-38; 3:19.) Hilo laweza kuonwa kwanza na mtu aliye na uhusiano wa karibu, kama vile mume akiona ushuhuda kama huo katika maoni na mwenendo wa mke wake aliyetengwa na ushirika. Hivyo aweza kuamua kwamba hakutenda ‘dhambi ya kufisha’ naye asukumwe katika kusali kwa ajili yake. Aweza kuomba kwamba ikiwa Yehova​—ajuaye yaliyo moyoni—​anaona msingi wa kumsamehe kosa lake, mapenzi ya Mungu yatendeke. Vilevile, anaweza kuonyesha Mungu tumaini lake kwamba mkewe apate nguvu kutokana na Biblia ili ashinde udhaifu wake.

Ijapokuwa huenda mtu akaona kwamba yeye binafsi aweza kumwendea Mungu kuhusiana na mtu ambaye ametengwa na ushirika, haingefaa kufanya hivyo mbele ya wengine au katika sala kundini. Inapaswa kufahamika kwamba wengine wanaosikia sala hiyo huenda wakawa bado hawajajua juu ya ushuhuda huo unaoonyesha toba. Au huenda wakawa hawajasadikishwa kwamba mtu huyo hakutenda “dhambi inayoleta kifo.”

Kwa hiyo, kuhusiana na hali ambayo katika hiyo Mkristo anaamini kwamba inafaa kusali kwa ajili ya mtu aliyetengwa na ushirika, apaswa kufanya hivyo katika sala za faraghani peke yake. Na sisi sote twaweza kujitahidi kuongoza kufikiri kwetu kuhusu jambo hili kulingana na shauri lililoongozwa kwa roho la Neno la Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki