Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 119
  • Neno la Mungu—Ni Nani au Ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Neno la Mungu—Ni Nani au Ni Nini?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Yohana 1:1—“Hapo Mwanzo Neno Alikuwako”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • Yule “Neno” Alikuwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • “Wale Wanaoitwa ‘Miungu’”
    Amkeni!—2005
  • Maandiko Husema Nini Juu ya “Uungu wa Kristo”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 119
Yesu akizungumza huku akiwa ameshika kitabu cha kukunjwa

Neno la Mungu—Ni Nani au Ni Nini?

Jibu la Biblia

Kwa kawaida, maneno “neno la Mungu” yanawakilisha ujumbe kutoka kwa Mungu au mkusanyo wa ujumbe huo. (Luka 11:28) Katika sehemu chache, “Neno la Mungu” au “Neno” hutumiwa kuwakilisha cheo cha mtu.​—Ufunuo 19:13; Yohana 1:​14.

Ujumbe kutoka kwa Mungu. Mara nyingi manabii walisema kwamba ujumbe ambao walitoa ulikuwa Neno la Mungu. Kwa mfano, Yeremia alianza ujumbe wake wa kinabii kwa kusema “neno la Yehova likaanza kunijia.” (Yeremia 1:4, 11, 13; 2:1) Kabla ya kumwambia Sauli kwamba Mungu alikuwa amemchagua kuwa mfalme, nabii Samweli alisema hivi: “Simama tuli sasa ili nikuambie neno la Mungu.”​—1 Samweli 9:27.

Cheo cha mtu. Pia “Neno” linaonekana katika Biblia likiwa cheo cha Yesu Kristo, akiwa roho mbinguni na pia akiwa mwanadamu duniani. Fikiria sababu kadhaa za kufikia mkataa huo:

  • Neno aliishi kabla ya vitu vingine vyote kuumbwa. “Hapo mwanzo Neno alikuwako . . . Hapo mwanzo huyo alikuwa pamoja na Mungu.” (Yohana 1:1, 2) Yesu ndiye “mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote . . . yeye ni wa kabla ya vitu vingine vyote.”​—Wakolosai 1:13-15, 17.

  • Neno alikuja duniani akiwa mwanadamu. “Neno akawa mwili, akakaa katikati yetu.” (Yohana 1:14) Kristo Yesu “alijiondolea mwenyewe hali yake na kuchukua umbo la mtumwa na kuwa kama wanadamu.”​—Wafilipi 2:5-7.

  • Neno ni Mwana wa Mungu. Baada ya kusema kwamba “Neno akawa mwili,” kama ilivyonukuliwa hapo juu, mtume Yohana aliendelea kusema hivi: “Nasi tukautazama utukufu wake, utukufu kama ule ulio wa mwana mzaliwa-pekee kutoka kwa baba.” (Yohana 1:14) Pia, Yohana aliandika hivi: “Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”​—1 Yohana 4:15.

  • Neno ana sifa kama za Mungu. “Neno alikuwa mungu.” (Yohana 1:1) Yesu “ndiye mng’ao wa utukufu [wa Mungu] na mwakilisho sawasawa wa utu wake wenyewe.”​—Waebrania 1:2, 3.

  • Neno anatawala akiwa mfalme. Biblia inasema kwamba kwenye kichwa cha Neno la Mungu “kuna vilemba vingi.” (Ufunuo 19:12, 13) Neno anaitwa pia “Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.” (Ufunuo 19:16) Yesu anaitwa “Mfalme wa wale wanaotawala wakiwa wafalme na Bwana wa wale wanaotawala wakiwa mabwana.”​—1 Timotheo 6:14, 15.

  • Neno ni msemaji wa Mungu. Inaonekana kwamba jina la cheo “Neno” linamtambulisha yule ambaye Mungu humtumia kuwasilisha habari na maagizo. Yesu alisema kwamba alitimiza jukumu hilo: “Baba mwenyewe aliyenituma amenipa amri kuhusu jambo la kutangaza na la kusema. . . . Kwa hiyo mambo ninayosema, kama vile Baba alivyoniambia, ndivyo ninavyoyasema.”​—Yohana 12:49, 50.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki