Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 69
  • Kwa Nini Ninapaswa Kusali?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Ninapaswa Kusali?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sala ni nini?
  • Je, Mungu anasikiliza?
  • Ninaweza kusali kuhusu nini?
  • Mkaribie Mungu Kupitia Sala
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Jinsi Unavyoweza Kumkaribia Mungu
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 69
Msichana ameketi pembeni ya ziwa

VIJANA HUULIZA

Kwa Nini Ninapaswa Kusali?

Utafiti mmoja uliofanywa unaonyesha kwamba asilimia 80 ya vijana nchini Marekani husali, lakini ni nusu tu ya vijana hao ambao wanasali kila siku. Bila shaka, baadhi yao wanajiuliza hivi: ‘Je, kusali ni njia ya kutuliza akili, au kuna jambo lingine la ziada?’

  • Sala ni nini?

  • Je, Mungu anasikiliza?

  • Ninaweza kusali kuhusu nini?

  • Vijana wenzako wanasema nini

Sala ni nini?

Sala ni mawasiliano halisi na Muumba wa vitu vyote. Hebu fikiria maana ya jambo hilo! Yehova ni mkuu kuliko wanadamu katika kila njia, hata hivyo, “hayuko mbali na kila mmoja wetu.” (Matendo 17:27) Kwa kweli, Biblia ina mwaliko huu mzuri: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.”​—Yakobo 4:8.

Unaweza kumkaribia Mungu jinsi gani?

  • Njia moja ni kupitia sala​—hivyo ndivyo unavyozungumza na Mungu.

  • Njia nyingine ni kupitia kujifunza Biblia​—hivyo ndivyo Mungu “anavyozungumza” nawe.

Kuwasiliana kwa njia hiyo​—sala na kujifunza Biblia​—kutakusaidia kujenga urafiki imara na Mungu.

“Kuzungumza na Yehova​—kuwasiliana na Aliye Juu Zaidi ​—ni mojawapo ya mapendeleo makubwa zaidi ambayo wanadamu wanaweza kupata.”​—Jeremy.

“Kumweleza Yehova hisia zangu za ndani kupitia sala hufanya nihisi nipo karibu zaidi naye.”​—Miranda.

Je, Mungu anasikiliza?

Ingawa unamwamini Mungu​—na hata unasali kwake​—inaweza kuwa vigumu kukubali ukweli kwamba yeye husikiliza tunaposali. Hata hivyo, Biblia inamwita Yehova “msikiaji wa sala.” (Zaburi 65:2) Hata anakualika ‘utupe mahangaiko yako yote juu yake.’ Kwa nini? ‘Kwa sababu yeye anakujali.’​—1 Petro 5:7.

Jambo la kufikiria: Je, unatenga wakati wa kuzungumza na rafiki zako wa karibu kwa ukawaida? Unaweza kutenga wakati pia wa kuzungumza na Mungu. Zungumza naye kwa ukawaida kupitia sala, na utumie jina lake, Yehova, unapofanya hivyo. (Zaburi 86:​5-7; 88:9) Kwa kweli, Biblia inakualika ufanye hivyo inaposema hivi: “Salini bila kuacha.”​—1 Wathesalonike 5:​17.

“Sala ni mazungumzo kati yangu na Baba yangu wa mbinguni, yule ambaye ninammiminia moyo wangu wote.”​—Moises.

“Ninazungumza na Yehova kwa kina kuhusu mambo, kama ambavyo ningefanya ninapozungumza na mama au rafiki yangu wa karibu sana.”​—Karen.

Ninaweza kusali kuhusu nini?

Biblia inasema hivi: “Katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu.”​—Wafilipi 4:6.

Je, hilo linamaanisha kwamba ni SAWA kusali kuhusu matatizo yako? Ndiyo! Kwa kweli, Biblia inasema hivi: “Mtupie Yehova mzigo wako, naye mwenyewe atakutegemeza.”​—Zaburi 55:22.

Bila shaka, unaposali kwa Mungu, unapaswa kumweleza mambo mengine zaidi ya matatizo yako tu. “Hautakuwa urafiki mzuri ikiwa nitamwomba Yehova msaada tu,” anasema mwanamke kijana anayeitwa Chantelle. “Ninahisi kwamba jambo la kwanza ni kumshukuru, na mambo ya kumshukuru yanapaswa kuwa mengi.”

Jambo la kufikiria: Ungependa kumshukuru Mungu kuhusu mambo gani katika maisha yako? Je, unaweza kufikiria mambo matatu ya kumshukuru Yehova leo?

“Hata mambo madogo kama vile kuvutiwa na ua zuri, yanaweza kukuchochea kusali ili umshukuru Yehova.”​—Anita

“Tafakari kuhusu kitu fulani katika uumbaji wa Yehova kinachokuvutia au mstari wa Biblia ambao kwa kweli unakugusa moyo, na kisha umshukuru Yehova kwa sababu ya mambo hayo.”​—Brian.

Vijana wenzako wanasema nini

Moises

“Kina cha sala zako kinapaswa kuwa kama kina cha bahari na si kama kidimbwi. Yehova anataka kutusaidia, na ingawa anajua mambo tunayohitaji hata kabla ya kumwomba, tunaweza kuonyesha jinsi tunavyomtumaini kwa kina cha sala zetu.”​—Moises.

Miranda

“Sala ni kama kamba ambayo Yehova ameshika upande mmoja nami nimeshika upande ule mwingine. Ninaposali kuhusu mambo yaliyo ndani ya moyo wangu, ninahisi ni kana kwamba ninaishika kamba hiyo kwa nguvu na Yehova pia anafanya hivyo, na hilo hufanya muungano wetu uwe imara.”​—Miranda.

Jeremy

“Tusipokuwa waangalifu, sala zetu zinaweza kuwa kama orodha ya mambo tunayotarajia atufanyie. Lakini tukimshukuru Yehova, tunaonyesha tunathamini mambo mengi anayotupatia na hatutajikazia uangalifu sana tunaposali bali tutakazia mambo mengine.”​—Jeremy.

Shelby

“Kadiri tunavyomshukuru Yehova, ndivyo tutakavyozidi kuwa wenye shukrani. Kumshukuru Yehova katika sala hutusaidia kukazia fikira baraka tunazopokea badala ya matatizo yote tunayokabili.”​—Shelby

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki