Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 137
  • Inamaanisha Nini Kuwa Mtakatifu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Inamaanisha Nini Kuwa Mtakatifu?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Je, mtu ambaye si mkamilifu anaweza kuwa mtakatifu?
  • Je, mtu anaweza kupoteza msimamo wa utakatifu mbele za Mungu?
  • Maoni yasiyo sahihi kuhusu kuwa mtakatifu
  • “Lazima Muwe Watakatifu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Je, Unayaona Mambo Matakatifu Kama Yehova Anavyoyaona?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • “Mimi Yehova Mungu Wenu Ni Mtakatifu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Kuitambua Roho Takatifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 137
Musa na kichaka cha miiba kinachowaka moto

Inamaanisha Nini Kuwa Mtakatifu?

Jibu la Biblia

Kuwa mtakatifu kunarejelea hali ya kutengwa na uchafuzi. Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “mtakatifu” linatokana na neno linalomaanisha “kutengwa.” Hivyo, kitu kitakatifu kimetengwa kutokana na matumizi ya kawaida, hasa kwa msingi wa kwamba ni safi na kimetakata.

Mungu ni mtakatifu kwa njia isiyo na kifani. Biblia inasema hivi: “Hakuna aliye mtakatifu kama Yehova.”a (1 Samweli 2:2) Basi inafaa kwamba Mungu ndiye huweka kiwango cha utakatifu.

Neno “takatifu” linaweza kutumiwa kurejelea chochote kinachohusianishwa na Mungu, hasa vitu ambavyo vimetengwa vitumiwe tu katika ibada. Kwa mfano, Biblia inazungumza kuhusu:

  • Maeneo matakatifu: Mungu alimwambia Musa hivi karibu na kichaka kilichokuwa kikiwaka moto: “Mahali unaposimama ni ardhi takatifu.”​—Kutoka 3:2-5.

  • Matukio matakatifu: Waisraeli wa kale walimwabudu Yehova wakati wa sherehe za kidini zilizofanywa kwa ukawaida zilizoitwa “makusanyiko matakatifu.”​—Mambo ya Walawi 23:37.

  • Vitu vitakatifu: Vitu vilivyotumiwa katika ibada ya Mungu kwenye hekalu la zamani kule Yerusalemu viliitwa ‘vyombo vitakatifu.’ (1 Wafalme 8:4) Vifaa hivyo vitakatifu vilipaswa kutendewa kwa heshima kubwa, ingawa havikupaswa kuabudiwa kamwe.b

Je, mtu ambaye si mkamilifu anaweza kuwa mtakatifu?

Ndiyo. Mungu anawaamuru Wakristo: “Lazima muwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu.” (1 Petro 1:16) Bila shaka, wanadamu wasio wakamilifu hawawezi kamwe kufikia kiwango kikamilifu cha Mungu cha utakatifu. Hata hivyo, wanadamu wanaotii sheria za uadilifu za Mungu wanaweza kuonekana kuwa ‘watakatifu na wenye kukubalika kwa Mungu.’ (Waroma 12:1) Mtu anayejitahidi kuwa mtakatifu anaonyesha hivyo kupitia maneno na matendo yake. Kwa mfano, anafuata shauri la Biblia linalosema kwamba tunapaswa ‘kuwa watakatifu na kujiepusha na uasherati’ na kwamba pia tunapaswa ‘kuwa watakatifu katika mwenendo wetu wote.’—1 Wathesalonike 4:3; 1 Petro 1:15.

Je, mtu anaweza kupoteza msimamo wa utakatifu mbele za Mungu?

Ndiyo. Mtu akiacha kufuata viwango vya Mungu vya mwenendo, Mungu hawezi kuendelea kumwona mtu huyo kuwa mtakatifu. Kwa mfano, kitabu cha Biblia cha Waebrania kinaelekezwa kwa “ndugu watakatifu,” hata hivyo, kinaonya kwamba wanaweza kusitawisha “moyo mwovu unaokosa imani . . . kwa kujiondoa kwa Mungu aliye hai.”​—Waebrania 3:1, 12.

Maoni yasiyo sahihi kuhusu kuwa mtakatifu

Maoni yasiyo sahihi: Mtu anaweza kuwa mtakatifu kwa kujinyima vitu fulani.

Ukweli: Biblia inafunua kwamba ‘kuutendea mwili kwa ukali, hakuna thamani yoyote’ kwa Mungu. (Wakolosai 2:23) Badala yake, Mungu anataka tufurahie vitu vizuri. “Kila mtu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yake yote ngumu. Ni zawadi kutoka kwa Mungu.”​—Mhubiri 3:13.

Maoni yasiyo sahihi: Useja humfanya mtu awe mtakatifu zaidi.

Ukweli: Ingawa Mkristo anaweza kuamua kuishi bila kufunga ndoa, useja haumfanyi mtu awe na mtakatifu mbele za Mungu. Ni kweli kwamba wale wanaoendelea kuwa waseja wanaweza kukazia fikira ibada yao bila kukengeshwa. (1 Wakorintho 7:32-34) Hata hivyo, Biblia inaonyesha kwamba wale ambao wamefunga ndoa wanaweza pia kuwa watakatifu. Kwa kweli, angalau mmoja wa mitume wa Yesu​—Petro​—alikuwa amefunga ndoa.​—Mathayo 8:14; 1 Wakorintho 9:5.

Maneno “Biblia Takatifu” yalitoka wapi?

Kwa karne nyingi, mkusanyo wote wa maandishi yaliyoongozwa na roho yameitwa “Biblia Takatifu” au “Maandiko Matakatifu” kwa sababu zifuatazo:

  • Chanzo chake. “Wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.”​—2 Petro 1:21.

  • Ujumbe wake. “Amri ya Yehova ni safi, huyafanya macho yang’ae. Kumwogopa Yehova ni jambo safi, hudumu milele.”​—Zaburi 19:8, 9.

Hivyo, Biblia inaweza kuonwa kuwa takatifu. Ni tofauti na maandishi mengine kwa sababu ya ujumbe wake safi na matumizi yake matakatifu katika ibada.

a Yehova ndilo jina la kibinafsi la Mungu. Katika mistari mingi sana ya Biblia jina hilo linahusianishwa na maneno “takatifu” na “utakatifu.”

b Biblia inashutumu matumizi ya sanamu za kidini katika ibada.​—1 Wakorintho 10:14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki