Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 138
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Dinosa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Dinosa?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1991
  • Kuutazama Ulimwengu
    Amkeni!—2006
  • Wanyama Humtukuza Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 138
Dinosa

Biblia Inasema Nini Kuhusu Dinosa?

Jibu la Biblia

Dinosa hawatajwi moja kwa moja katika Biblia. Hata hivyo, Biblia inasema kwamba Mungu ndiye ‘aliumba vitu vyote,’ kwa hiyo, ni wazi kwamba dinosa walikuwa miongoni mwa vitu alivyoumba.a (Ufunuo 4:​11) Bila kutaja dinosa kihususa, Biblia inataja vikundi vifuatavyo vya viumbe ambavyo huenda vilitia ndani dinosa:

  • “Viumbe wakubwa wa baharini.”​—Mwanzo 1:21.

  • “Wanyama wote wanaotambaa.”​—Mwanzo 1:​25.

  • “Wanyama wa mwituni.”​—Mwanzo 1:​25.

Je, dinosa walitokana na wanyama wengine kupitia mageuzi?

Rekodi ya vitu vya kale vilivyochimbuliwa inaonyesha kwamba badala ya kutokea hatua kwa hatua kana kwamba kwa mageuzi, dinosa walikuwepo duniani wakati uleule mmoja. Hilo linapatana na ujumbe wa Biblia unaoonyesha kwamba Mungu aliumba wanyama wote. Kwa mfano, Zaburi 146:6 inamwonyesha Mungu kuwa “Muumba wa mbingu na dunia, wa bahari, na vyote vilivyomo.”

Dinosa waliishi wakati gani?

Biblia inaonyesha kwamba wanyama wa baharini na wa nchi kavu waliumbwa katika siku ya tano na ya sita ya uumbaji.b (Mwanzo 1:​20-​25, 31) Hivyo, Biblia inaonyesha kwamba huenda dinosa waliumbwa na kuendelea kuwepo kwa muda mrefu.

Je, Behemothi na Lewiathani walikuwa dinosa?

Hapana. Ingawa hatuwezi kuwatambulisha wanyama wanaotajwa katika kitabu cha Ayubu kwa uhakika, kwa kawaida Behemothi anatambulishwa kuwa kiboko na Lewiathani kuwa mamba. Utambulisho huo unapatana na ufafanuzi kuwahusu unaopatikana katika Maandiko. (Ayubu 40:15-​23; 41:​1, 14-​17, 31) Vyovyote vile, maneno “Behemothi” na “Lewiathani” hayawezi kurejelea dinosa. Sababu ni kwamba Mungu alimwambia Ayubu awatazame wanyama hao, naye Ayubu aliishi muda mrefu sana baada ya dinosa kutoweka duniani.​—Ayubu 40:16; 41:8.

Kwa nini dinosa walitoweka?

Biblia haielezi jinsi dinosa walivyotoweka. Hata hivyo, inasema kwamba kila kitu kiliumbwa “kwa sababu ya mapenzi” ya Mungu, kwa hiyo, ni wazi kwamba Mungu alikuwa na kusudi la kuumba dinosa. (Ufunuo 4:​11) Kusudi hilo lilipotimia, Mungu aliruhusu dinosa watoweke.

a Rekodi ya vitu vya kale vilivyochimbuliwa inathibitisha kwamba dinosa walikuwepo. Vitu hivyo vya kale vinaonyesha kwamba kuna wakati ambapo kulikuwa na dinosa wengi sana wenye maumbo na ukubwa mbalimbali.

b Katika Biblia, neno “siku” linaweza kurejelea vipindi vya wakati vinavyodumu kwa maelfu ya miaka.​—Mwanzo 1:​31; 2:​1-4; Waebrania 4:​4, 11.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki