Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 8/15 uku. 3
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • “Taifa” Linalolisha Mamilioni ya Watu Wenye Njaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Mkono wa Yehova Wainuliwa
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Wokovu kwa Wanaochagua Nuru
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Ikiwa Mungu Ana Tengenezo, Ni Tengenezo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 8/15 uku. 3

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Ni nani au ni nini kinachofananishwa na “Leviathani” wa Isaya 27:1, NW?

Andiko la Isaya 27:1 (NW) linasomwa hivi: “Katika siku hiyo Yehova, kwa upanga wake mgumu ulio mkuu na wenye nguvu, atageuza fikira zake kwenye Leviathani, yule nyoka anayenyiririka, hata kwenye Leviathani, yule nyoka mwenye kupotoka-potoka, na yeye kwa uhakika ataua lile dubwana la bahari lililo katika ile bahari.” Sisi tunauelewa unabii huu , kuwa unahusu Shetani Ibilisi na pia tengenezo lake bovu duniani.

Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 15, 1985, ulieleza kwamba Isaya 27 ni unabii wa kurudishwa. Utimizo wao wa kwanza ulilihusu taifa la kale la Israeli, ambalo lingerudishwa kwenye nchi yalo ya nyumbani baada ya kuwa mateka miaka 70 katika Babuloni. Ingawa walio wengi kati ya wahamishwa wangekuja kutoka Babuloni, wengine wangerudi kutoka Misri na eneo la Ashuru. Yehova Mungu aliazimia kwamba watu wake wamepaswa kuachwa huru, kwa hiyo mataifa hayo hayangeweza kumzuia kupitia jitihada za kujitegemea wenyewe au za muungano. Kwa wanadamu huenda ikawa yalionekana kama kwamba yalikuwa yenye nguvu nyingi na ulaghai, kama Leviathani wa kale (labda huyo akiwa ni mamba), hata hivyo, Yehova angefanikiwa katika hatua yake kwa ajili ya Israeli wa kale.​—Linganisha Ayubu 41:1-34.

Ingawa hivyo, “Leviathani” angefananisha nini katika utimizo mkubwa zaidi wa Isaya 27? Kwa wazi, wazo linaingia akilini kwamba anayemaanishwa ni Shetani Ibilisi, kwa maana Ufunuo 12:9 unamweleza yeye kuwa ‘yule joka mkubwa’ na “nyoka wa zamani.” Kwa muda mrefu amekuwa adui wa mungu na watu Wake. Zaidi ya hilo, Maandiko yanaonyesha wazi kwamba Shetani atafikia mwisho wake. Mungu ameweka siku ya kutumia uwezo wake kupitia Mwanaye ili amwondoe Ibilisi. Kwa hiyo huyo “joka” au “nyoka” ataangushwa chini kwa kukatwa kama kwamba ni kwa upanga mkubwa ulio na nguvu.​—Waebrania 2:14; Ufunuo 20:1-3, 10.

Lakini kumbuka kwamba adui za karibu waliokabili Israeli wa kale ni mataifa yenye kuonekana yaliyokuwa na upinzani, kama vile Misri, Ashuru, na Babuloni. Vivyo hivyo, leo watumishi wa Kikristo wa Mungu ulimwenguni pote wanakabiliwa na wapinzani wenye kuonekana katikati ya bahari isiyotulia ya wanadamu waliotengwa wakawa mbali na Mungu. (Ufunuo 17:1, 15) Shetani anaongoza tengenezo la ulimwenguni pote analotumia ili kuwazuia njia wale “wazishikao amri za Mungu na kuwa na ushuhuda wa Yesu.” (Ufunuo 12:17) Tengenezo hilo lenye kutawalwa na Ibilisi limethibitika kuwa lenye ujanja na ukali, kama leviathani. Hata hivyo, mapema katika karne hii “Leviathani” huyo alipoteza uongozi wake juu ya Israeli wa kiroho, yaani, wale mashahidi Wakristo waliopakwa mafuta wa Yehova. Naye ataangushwa kabisa kwa kukatwa wakati Yesu, akiwa amefuatwa na malaika walio mashujaa wa kivita, akiwa amepanda farasi na kusonga mbele kwa kushika ‘upanga mkali ili awapige mataifa kwa huo.’​—Ufunuo 19:11-16.

Kwa hiyo ingawa kwa upande mmoja Shetani anaweza kusemwa kuwa ndiye yule Leviathani wa Isaya 27:1, unabii huo unatia ndani wengi zaidi ya yule “nyoka wa zamani” tu. Unakaza fikira hasa juu ya tengenezo la kidunia lenye kuonekana linaloongozwa naye. Hivyo, Mnara wa Mlinzi uliotangulia kutajwa ungeweza kuelekeza wasomaji kwenye wakati ambao “mfumo mbovu wa sasa ambao Shetani Ibilisi ameutawala akiwa mungu wao, hautakuwako. Yehova atakuwa amekwisha kuelekeza fikira zake kwenye yule Leviathani wa mfano, yule nyoka mwenye kujinyiririsha, mwenye kupotoka-potoka, aliyemo katikati ya bahari ambayo ni wanadamu. Yeye na mataifa, na hata miungano ya mataifa, watakwisha.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki