Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwhf makala 1
  • Jinsi ya Kudhibiti Hasira

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kudhibiti Hasira
  • Msaada kwa Ajili ya Familia
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Hasira?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je! Ni Vibaya Nyakati Zote Kuwa na Hasira?
    Amkeni!—1994
  • Hasira—Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Hasira
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Msaada kwa Ajili ya Familia
ijwhf makala 1
Mke akiwa amekasirika kwa kuwa mume anatazama televisheni huku yeye akiosha vyombo

MSAADA KWA AJILI YA FAMILIA

Jinsi ya Kudhibiti Hasira

Mwenzi wako anasema jambo ambalo linakukasirisha, na unajaribu kufungia hasira yako. Lakini mwenzi wako anahisi kwamba amekukosea kwa njia fulani, kwa hiyo anaanza kukuhoji. Kufanya hivyo kunakukasirisha zaidi. Unaweza kufanya nini ili udhibiti hasira yako chini ya hali kama hizo?

  • Mambo unayohitaji kujua

  • Mambo unayoweza kufanya

Mambo unayohitaji kujua

  • Kukasirika kunaweza kudhuru afya yako. Utafiti unaonyesha kwamba hasira isipodhibitiwa inaongeza hatari ya kupanda kwa shinikizo la damu, kupata ugonjwa wa moyo, kushuka moyo, na matatizo ya umeng’enyaji. Pia, hasira imehusianishwa na matatizo ya kukosa usingizi, kuongezeka kwa mahangaiko, matatizo ya ngozi, na kiharusi. Inafaa kwamba Biblia inasema hivi: “Usikasirike, kwa maana hasira itakuongoza tu kwenye madhara.”​—Zaburi 37:8, maelezo ya chini.

  • Kufungia hasira kunaweza kukudhuru pia. Ukiendelea kufungia hasira inaweza kuwa kama ugonjwa ambao unakuumiza kutokea ndani. Kwa mfano, unaweza kuwa na mtazamo wa kuona tu mambo mabaya na kuchambua-chambua. Roho kama hiyo inaweza kufanya iwe vigumu kuishi pamoja nawe na kuathiri sana ndoa yako.

Mambo unayoweza kufanya

  • Tafuta sifa nzuri za mwenzi wako. Orodhesha mambo matatu unayopenda kumhusu mwenzi wako. Wakati ujao utakapokasirishwa na kitu ambacho mwenzi wako anafanya, fikiria kuhusu sifa hizo ulizotaja. Huenda hilo likakusaidia kudhibiti hasira yako.

    Kanuni ya Biblia: “Mjionyeshe kuwa wenye shukrani.”​—Wakolosai 3:15.

    Mke mwenye shughuli nyingi anafikiria jinsi mume wake humsaidia kufanya kazi za nyumba, kumsikiliza, na kumjali anapokuwa mgonjwa
  • Sitawisha mtazamo wa kusamehe. Kwanza, jaribu kuona mambo kwa kutegemea maoni ya mwenzi wako. Hilo litakusaidia uwe na hisia kama za mwenzi wako​—Biblia inasema kufanya hivyo ni kusitawisha “hisia-mwenzi.” (1 Petro 3:8) Kisha jiulize, ‘Je, jambo linalonifanya nikasirike ni kubwa sana hivi kwamba siwezi kusamehe?’

    Kanuni ya Biblia: “Ni fahari . . . kuachilia kosa.”​—Methali 19:11.

  • Eleza hisia zako kwa fadhili na busara. Jieleze ukitumia neno “mimi.” Kwa mfano, badala ya kusema, “Wewe unakosa ufikirio unapokosa kunipigia simu na kunijulisha mahali ulipo,” sema “Mimi huwa na wasiwasi saa zinaposonga na sijui ikiwa uko salama.” Kueleza hisia zako kwa upole kunaweza kukusaidia kudhibiti hasira yako.

    Kanuni ya Biblia: “Maneno yenu na yawe yenye neema sikuzote, yaliyokolezwa chumvi.”​—Wakolosai 4:6.

  • Sikiliza kwa heshima. Baada ya kujieleza, mruhusu mwenzi wako azungumze bila kumkatiza. Mwenzi wako anapomaliza kuzungumza, rudia kwa maneno machache kile alichosema ili uone ikiwa umemwelewa vizuri. Tendo dogo la kusikiliza linaweza kuchangia sehemu kubwa katika kukusaidia kudhibiti hasira yako.

    Kanuni ya Biblia: ‘Uwe mwepesi wa kusikia, si mwepesi wa kusema.’​—Yakobo 1:​19.

Tim na Jennifer

“Ukifungia hasira, tatizo litaendelea kujirudia na mwishowe utalipuka. Ni afadhali kuzungumzia tatizo hilo kwa heshima. Baada ya kuzungumza, mimi na mume wangu hupenda kuambiana, ‘Acha turudi kuwa marafiki tena.’”​—Jennifer, akiwa na mume wake, Tim.

Jade na Corey

“Jambo moja ambalo ninathamini kumhusu mume wangu ni kwamba sikuzote yeye hunisikiliza na kuheshimu mambo yanayonihangaisha. Hata ikiwa hakubaliani nami, yeye hufikiria maoni yangu. Hakuna wakati anaponifanya nijihisi mjinga kwa sababu ya hisia zangu.”​—Jade, akiwa na mume wake, Corey.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki