Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 144
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Kuchoma Maiti?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Kuchoma Maiti?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Maoni yasiyo sahihi kuhusu kuchoma maiti
  • Je, Ni Vibaya Kuteketeza Maiti?
    Amkeni!—2009
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Kurudi Mavumbini—Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Yaliyomo
    Amkeni!—2009
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 144
Chupa iliyo na majivu ya maiti iliyochomwa ikiwa kando ya picha ya aliyekufa

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kuchoma Maiti?

Jibu la Biblia

Biblia haitoi mwongozo wowote hususa kuhusu desturi ya kuchoma maiti. Hakuna amri yoyote katika Biblia kuhusu kuzika au kuchoma maiti.

Biblia inaripoti pindi ambazo watumishi waaminifu wa Mungu walizika maiti za wapendwa wao. Kwa mfano, Abrahamu alifanya jitihada kubwa ili kupata sehemu ya kumzika mke wake, Sara.​—Mwanzo 23:​2-​20; 49:29-​32.

Pia, Biblia inataja watu fulani waaminifu ambao walichoma maiti. Kwa mfano, Mfalme Sauli wa Israeli na wana wake watatu walipouawa vitani, mwanzoni maiti zao zilibaki katika eneo la maadui na zilitendewa kwa njia isiyo ya heshima. Mashujaa waaminifu wa Israeli waliposikia kuhusu hilo, walienda kuichukua miili ya Sauli na wana wake, wakaiteketeza na kuzika mabaki yake. (1 Samweli 31:​8-​13) Biblia inaonyesha kwamba hiyo ilikuwa njia inayokubalika ya kushughulikia maiti za wanaume hao.​—2 Samweli 2:​4-6.

Maoni yasiyo sahihi kuhusu kuchoma maiti

Maoni yasiyo sahihi: Kuchoma maiti hushushia heshima mwili.

Ukweli: Biblia inasema kwamba wale wanaokufa hurudi mavumbini, na hilo ndilo jambo la asili ambalo hupata maiti inapooza. (Mwanzo 3:​19) Kuchoma maiti huharakisha jambo hilo kwa kufanya mwili uwe majivu, au vumbi.

Maoni yasiyo sahihi: Katika nyakati za Biblia, maiti za watu ambao hawakuwa na kibali cha Mungu ndizo zilizochomwa baada ya wao kufa.

Ukweli: Maiti za watu fulani ambao hawakuwa waaminifu, kama vile Akani na familia yake, zilichomwa. (Yoshua 7:​25) Lakini haikuwa kawaida kufanya hivyo. (Kumbukumbu la Torati 21:22, 23) Kama ilivyotajwa mapema, maiti za watu fulani waaminifu, kama vile Yonathani, mwana wa Mfalme Sauli, zilichomwa walipokufa.

Maoni yasiyo sahihi: Kuchoma maiti kunamzuia Mungu kumfufua mtu.

Ukweli: Kuhusu ufufuo wa wafu, si jambo kubwa kwa Mungu ikiwa mwili wa mtu ulizikwa, ulichomwa, ulipotea baharini, au uliliwa na wanyama wa mwituni. (Ufunuo 20:13) Mweza-Yote anaweza kumuumbia mtu huyo mwili mpya kwa urahisi.​—1 Wakorintho 15:35, 38.

Utaamuaje Ikiwa Uchome Maiti au Uizike?

Unapofanya uamuzi wa kushughulikia maiti, fikiria mambo yafuatayo.

  • Mapendezi ya aliyekufa. Biblia inarekodi pindi ambapo washiriki wa familia waliheshimu maombi ambayo mtu alitoa alipokuwa hai kuhusu jinsi ya kushughulikia mwili wake atakapokufa.​—Mwanzo 50:​4, 5; Kutoka 13:19.

  • Desturi za kwenu. Mara nyingi desturi huamua jinsi mwili utakavyoshughulikiwa. (Yohana 19:40) Kwa mfano, katika nyakati za Biblia, ilikuwa kawaida kuzika waliokufa. (Mwanzo 49:31; 1 Samweli 28:3) Vivyo hivyo leo, mtu anaweza kuamua kushughulikia maiti kupatana na desturi za eneo, maadamu desturi hizo hazipingani na kanuni za Biblia.

  • Matakwa ya kisheria. Biblia inawatia watu moyo watii mamlaka za serikali. (Waroma 13:1) Katika maeneo fulani, wenye mamlaka huweka sheria ya jinsi ya kushughulikia maiti. Kwa mfano, kuhusu kuchoma maiti, wenye mamlaka huweka vizuizi vya mahali ambapo majivu yanaweza kutupwa.

  • Hisia za wengine. Maandiko yanatutia moyo tufikirie faida za wengine. (Wafilipi 2:4) Tunapoamua jinsi ya kushughulikia maiti, tunahitaji kufikiria maswali yafuatayo: Watu wengine wa familia wanahisije kuhusu kuchoma maiti au kuzika mwili wake? Jamii inaonaje desturi kama hizo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki