Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 155
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutoa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutoa?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Ni wakati gani ambapo Mungu anafurahi tunapotoa?
  • Ni wakati gani ambapo Mungu hafurahi tunapotoa?
  • “Mungu Hupenda Mtoaji Mchangamfu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Je, Una Roho ya Kutoa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Yehova Huwapenda Watoaji Wachangamfu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Furahia Faida za Kuwa Mkarimu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 155
Mtu akiwa ameshika boksi lenye zawadi

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutoa?

Jibu la Biblia

Biblia inatutia moyo kutoa kwa hiari na kwa nia nzuri. Inaonyesha kwamba kutoa kwa njia hiyo kunamnufaisha anayepokea na anayetoa pia. (Methali 11:25; Luka 6:38) Yesu alisema hivi: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”​—Matendo 20:35.

  • Ni wakati gani ambapo Mungu anafurahi tunapotoa?

  • Ni wakati gani ambapo Mungu hafurahi tunapotoa?

  • Maandiko yanayohusu kutoa

Ni wakati gani ambapo Mungu anafurahi tunapotoa?

Mungu anafurahi tunapotoa kwa hiari. Biblia inasema hivi: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si bila kutaka wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu.”​—2 Wakorintho 9:7, maelezo ya chini.

Kutoa kwa hiari ni “namna ya dini” ambayo Mungu anakubali. (Yakobo 1:27, maelezo ya chini) Mtu anayewasaidia wengine kwa ukarimu anafanya kazi pamoja na Mungu, ambaye anaona ukarimu huo kuwa mkopo kwake. (Methali 19:17) Biblia inafundisha kwamba Mungu atamlipa yule anayetoa.​—Luka 14:12-​14.

Ni wakati gani ambapo Mungu hafurahi tunapotoa?

Tunapotoa kwa nia mbaya. Ifuatayo ni mifano kadhaa:

  • Ili tusifiwe na watu.​—Mathayo 6:2.

  • Ili tulipwe kwa njia fulani.​—Luka 14:12-14.

  • Ili tujaribu kununua wokovu.​—Zaburi 49:6, 7.

Ikiwa zawadi yetu itatumiwa kuunga mkono utendaji na mitazamo ambayo Mungu anashutumu. Kwa mfano, lingekuwa kosa kumpa mtu pesa za kucheza kamari au kutumia kileo vibaya au dawa za kulevya. (1 Wakorintho 6:9, 10; 2 Wakorintho 7:1) Vivyo hivyo, si sawa kumpa mtu ambaye anaweza kujitegemeza lakini anakataa kufanya kazi.​—2 Wathesalonike 3:​10.

Wakati ambapo kutoa kunaingilia majukumu tuliyopewa na Mungu. Biblia inafundisha kwamba vichwa vya familia wanapaswa kuandaa mahitaji ya familia zao. (1 Timotheo 5:8) Si jambo linalofaa kwa kichwa cha familia kuwapa wengine kupita kiasi hivi kwamba familia yake inateseka. Vivyo hivyo, Yesu aliwashutumu wale waliokataa kuwaandalia wazazi wao waliozeeka kwa kudai kwamba mali zao zote zilikuwa “zawadi iliyowekwa wakfu kwa Mungu.”​—Marko 7:​9-​13.

Maandiko yanayohusu kutoa

Methali 11:25: “Mtu mkarimu atapata ufanisi, na yule anayewaburudisha wengine yeye mwenyewe ataburudishwa.”

Maana: Kutoa humnufaisha anayepokea na anayetoa.

Methali 19:17: “Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova, naye Atamlipa kwa anayotenda.”

Maana: Mungu anaona kwamba ana deni kwa wale wanaowasaidia wenye uhitaji, na anaahidi kuwalipa kwa ukarimu wao.

Mathayo 6:2: “Unapotoa zawadi za rehema, usipige tarumbeta mbele yako kama wanavyofanya wanafiki . . . ili wasifiwe na watu.”

Maana: Hatupaswi kutoa ili watu watutambue.

Matendo 20:35: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”

Maana: Ukarimu unaotoka moyoni huleta furaha.

2 Wakorintho 9:7: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu.”

Maana: Kutoa kwa hiari humfurahisha Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki