Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 157
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Misiba ya Asili?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Misiba ya Asili?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba misiba ya asili si adhabu kutoka kwa Mungu?
  • Je, misiba ya asili ni ishara ya nyakati?
  • Mungu anawasaidiaje waathiriwa wa misiba ya asili?
  • Je, Biblia inaweza kutusaidia kujitayarisha kwa ajili ya misiba?
  • Misiba ya Asili​—Kwa Nini Imeongezeka Sana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Je, Misiba ya Asili Ni Adhabu Kutoka Kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Je, Mungu Anatumia Misiba ya Asili Kuwaadhibu Wanadamu Leo?
    Amkeni!—2012
  • Misiba ya Asili-Je! Mungu Ndiye Huisababisha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 157
Familia ikitazama mtaa ulioharibiwa na msiba wa asili

Biblia Inasema Nini Kuhusu Misiba ya Asili?

Jibu la Biblia

Mungu hasababishi misiba ya asili inayotokea leo, lakini anawajali watu wanaoathiriwa na misiba hiyo. Ufalme wa Mungu utakomesha mambo yote yanayotufanya tuteseke, kutia ndani misiba ya asili. Kwa sasa, Mungu anaandaa faraja kwa wale walioathiriwa na misiba ya asili.​—2 Wakorintho 1:3.

  • Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba misiba ya asili si adhabu kutoka kwa Mungu?

  • Je, misiba ya asili ni ishara ya nyakati?

  • Mungu anawasaidiaje waathiriwa wa misiba ya asili?

  • Je, Biblia inaweza kutusaidia kujitayarisha kwa ajili ya misiba ya asili?

  • Mistari ya Biblia inayoweza kuwafariji waathiriwa wa misiba ya asili

Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba misiba ya asili si adhabu kutoka kwa Mungu?

Misiba ya asili inatofautiana na jinsi Mungu anavyotumia nguvu za asili kama inavyotajwa katika Biblia.

  • Misiba ya asili huua na kuwajeruhi watu bila kuchagua. Tofauti na hilo, Mungu alipotumia nguvu za asili kutekeleza hukumu kama ilivyorekodiwa katika Biblia, alihakikisha kwamba ni waovu tu walioangamizwa. Kwa mfano, Mungu alipoharibu majiji ya kale ya Sodoma na Gomora, alihakikisha kwamba Loti na binti zake waliokoka. (Mwanzo 19:29, 30) Mungu alisoma mioyo ya watu wa wakati huo na kuwaharibu wale tu ambao aliwaona kuwa waovu.​—Mwanzo 18:23-32; 1 Samweli 16:7.

  • Mara nyingi misiba ya asili hutokea bila kutoa onyo. Kwa upande mwingine, Mungu aliwaonya waovu kabla ya kutumia nguvu za asili dhidi yao. Watu waliotii maonyo hayo walipata nafasi ya kuponyoka.​—Mwanzo 7:​1-5; Mathayo 24:38, 39.

  • Kwa kadiri fulani, wanadamu wamechangia kutokea kwa misiba ya asili. Jinsi gani? Kwa kuharibu mazingira na kujenga katika maeneo ambako matetemeko ya ardhi, mafuriko, na hali mbaya sana ya hewa hutokea kwa ukawaida. (Ufunuo 11:18) Mungu hapaswi kulaumiwa kwa sababu ya makosa ya wanadamu.​—Methali 19:3.

Je, misiba ya asili ni ishara ya nyakati?

Ndiyo, unabii wa Biblia unaonyesha kwamba kungekuwa na misiba wakati wa “umalizio wa mfumo wa mambo,” au katika “siku za mwisho.” (Mathayo 24:3; 2 Timotheo 3:1) Kwa mfano, kuhusu wakati wetu, Yesu alisema hivi: “Kutakuwa na upungufu wa chakula na matetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali.” (Mathayo 24:7) Hivi karibuni, Mungu atakomesha mambo yote yanayosababisha maumivu na kuteseka, kutia ndani misiba ya asili.​—Ufunuo 21:3, 4.

Mungu anawasaidiaje waathiriwa wa misiba ya asili?

  • Mungu huwafariji waathiriwa kwa kutumia Neno lake, Biblia. Biblia inatuhakikishia kwamba Mungu anatujali na kwamba anahuzunika tunapoteseka. (Isaya 63:9; 1 Petro 5:6, 7) Pia, anafunua ahadi yake ya wakati ambapo misiba ya asili haitakuwepo tena.​—Ona “Mistari ya Biblia inayoweza kuwafariji waathiriwa wa misiba ya asili.”

  • Mungu huwasaidia waathiriwa kupitia waabudu wake. Mungu huwatumia waabudu wake duniani kuiga mfano uliowekwa na Yesu. Ilitabiriwa kwamba Yesu angewafariji “waliovunjika moyo” na “wote wanaoomboleza.” (Isaya 61:1, 2) Waabudu wa Mungu wanajitahidi kufanya vivyo hivyo.​—Yohana 13:15.

    Pia, Mungu hutumia waabudu wake kuandaa msaada unaofaa kwa waathiriwa wa misiba ya asili.​—Matendo 11:28-30; Wagalatia 6:10.

Mashahidi wa Yehova wakirekebisha nyumba nchini Puerto Riko

Mashahidi wa Yehova wakiandaa msaada kwa ajili ya waathiriwa wa kimbunga nchini Puerto Riko

Je, Biblia inaweza kutusaidia kujitayarisha kwa ajili ya misiba?

Ndiyo. Ingawa Biblia haikuandikwa iwe mwongozo wa kujitayarisha ajili ya misiba, ina kanuni zinazoweza kutusaidia. Kwa mfano:

  • Panga mapema kwa ajili ya misiba inayoweza kutokea. Biblia inasema: “Mtu mwerevu huona hatari na kujificha.” (Methali 22:3) Ni jambo la hekima kutayarisha mapema kile tutakachofanya hali ya dharura inapotokea. Huenda matayarisho kama hayo yakahusisha kupanga mkoba wa dharura ambao umeandaliwa tayari na kupanga pamoja na familia mahali pa kukutana ikiwa msiba utatokea.

  • Uhai ni muhimu kuliko mali. Biblia inasema: “Hatukuleta chochote ulimwenguni, wala hatuwezi kuondoka na chochote.” (1 Timotheo 6:7, 8) Tunahitaji kuwa tayari kuacha nyumba na mali zetu ili kuokoka msiba. Tunapaswa kukumbuka kwamba uhai wetu ni muhimu zaidi kuliko vitu vyovyote vya kimwili.​—Mathayo 6:25.

Mistari ya Biblia inayoweza kuwafariji waathiriwa wa misiba ya asili

Mwanzo 18:25: “Ni jambo usiloweza [Mungu] kuwazia kumuua mwadilifu pamoja na mwovu . . . Je, Mwamuzi wa dunia yote hatatenda jambo la haki?”

Maana: Sikuzote Mungu hufanya kilicho sawa; hapaswi kulaumiwa watu wema wanapokufa kwa sababu ya misiba ya asili.

Zaburi 46:​1, 2: “Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, msaada unaopatikana kwa urahisi nyakati za taabu. Ndiyo sababu hatutaogopa, hata dunia ikibadilika.”

Maana: Hata nini kikitokea, tunaweza kumtegemea Mungu atuimarishe.

Isaya 63:9: “Katika taabu zao zote, yeye alitaabika.”

Maana: Mungu ana hisia-mwenzi​—anatuhurumia tunapoteseka.

Yohana 5:​28, 29: “Saa inakuja ambayo wote walio katika makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti [ya Yesu] na kutoka.”

Maana: Tunaweza kuwa na tumaini la kuwaona tena wapendwa wetu waliokufa kwa sababu Mungu atampa Yesu uwezo wa kuwafufua.

1 Petro 5:​6, 7: “Kwa hiyo, jinyenyekezeni chini ya mkono wenye nguvu wa Mungu, . . . huku mkitupa mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.”

Maana: Mungu anatujali sana na anataka tusali kwake kuhusu mahangaiko yetu.

Ufunuo 21:4: “[Mungu] atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”

Maana: Mungu ataondoa visababishi vyote vya kuteseka kutia ndani misiba ya asili.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki