Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbv makala 14
  • Methali 3:5, 6—“Usizitegemee Akili Zako Mwenyewe”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Methali 3:5, 6—“Usizitegemee Akili Zako Mwenyewe”
  • Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maana ya Methali 3:5 6
  • Muktadha wa Methali 3:5, 6
  • Mtumaini Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Methali 22:6—“Mlee Mtoto Katika Njia Impasayo”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • Hekima Kutoka kwa Mungu Inayotuongoza Maishani
    Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Uongozi Timamu kwa Vijana wa Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
ijwbv makala 14

MISTARI YA BIBLIA YAFAFANULIWA

Methali 3:5, 6—“Usizitegemee Akili Zako Mwenyewe”

“Mtumaini Yehova kwa moyo wako wote, wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Katika njia zako zote mtambue yeye, naye atavinyoosha vijia vyako.”—Methali 3:5, 6, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

“Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe. Katika njia zako zote mkiri yeye, naye atanyoosha mapito yako.”—Methali 3:5, 6, Union Version.

Maana ya Methali 3:5 6

Badala ya kujifanyia maamuzi yoyote muhimu, tunapaswa kutafuta mwongozo wa Yehovaa Mungu.

“Mtumaini Yehova kwa moyo wako wote.” Tunaonyesha kwamba tunamtumaini Mungu tunapofanya mambo kama yeye anavyoelekeza. Tunapaswa kumtumaini Mungu kikamili, kwa moyo wetu wote. Katika Biblia, mara nyingi moyo hurejelea mtu wa ndani, na hilo linahusisha hisia za mtu, mambo yanayomchochea, fikira, na mtazamo. Hivyo, kumtumaini Mungu kwa moyo wetu kunahusisha mengi zaidi ya hisia zetu. Ni uamuzi tunaofanya kwa sababu tumesadikishwa kabisa kwamba Muumba wetu anajua ni nini kinachotufaa zaidi.—Waroma 12:1.

“Usitegemee uelewaji wako mwenyewe.” Tunapaswa kumtumaini Mungu kwa sababu hatuwezi kutegemea maoni yetu yasiyokamilika. Ikiwa tutajitumaini kabisa au kuruhusu hisia zetu ziamue mambo tutakayofanya, tunaweza kufanya maamuzi ambayo mwanzoni huenda yanaonekana kuwa mazuri lakini mwishowe yakaleta matokeo mabaya. (Methali 14:12; Yeremia 17:9) Hekima ya Mungu ni bora zaidi kuliko yetu. (Isaya 55:8, 9) Tutafanikiwa sana maishani ikiwa tutaongozwa na Mungu.—Zaburi 1:1-3; Methali 2:6-9; 16:20.

“Katika njia zako zote mtambue yeye.” Tunapaswa kutafuta maoni ya Mungu katika kila jambo muhimu maishani mwetu na kila uamuzi muhimu tunaofanya. Tunafanya hivyo kwa kusali kwake tukimwomba atupatie mwongozo na kwa kufuata anachosema katika Neno lake, Biblia.—Zaburi 25:4; 2 Timotheo 3:16, 17.

“Atavinyoosha vijia vyako.” Mungu ananyoosha njia yetu kwa kutusaidia kuishi kulingana na viwango vyake vya uadilifu. (Methali 11:5) Hivyo, tunaepuka matatizo yoyote yasiyo ya lazima na kuwa na maisha yenye furaha.—Zaburi 19:7, 8; Isaya 48:17, 18.

Muktadha wa Methali 3:5, 6

Kitabu cha Biblia cha Methali kina kanuni za msingi zinazosaidia kuwa na maisha yenye furaha na mafanikio mbele za Mungu. Sura tisa za kwanza zimeandikwa kama ushauri wa baba kwa mtoto wake mpendwa. Sura ya 3 inataja manufaa wanayopata wale wanaothamini na kutumia hekima ya Muumba wetu.—Methali 3:13-26.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.—Zaburi 83:18.

Soma Methali sura ya 3 pamoja na ufafanuzi wa maelezo ya chini na marejeo ya maandiko mengine.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki