Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bm seh. ya 12 uku. 15
  • Hekima Kutoka kwa Mungu Inayotuongoza Maishani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hekima Kutoka kwa Mungu Inayotuongoza Maishani
  • Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Cha Biblia Namba 20—Mithali
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Uongozi Timamu kwa Vijana wa Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Methali 3:5, 6—“Usizitegemee Akili Zako Mwenyewe”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • Pata Hekima na Ukubali Nidhamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Biblia—Ina Ujumbe Gani?
bm seh. ya 12 uku. 15
Watu katika nyakati za Biblia wakikusanya nafaka

Sehemu ya 12

Hekima Kutoka kwa Mungu Inayotuongoza Maishani

Kitabu cha Methali ni hazina ya mashauri kutoka kwa Mungu yanayotupa mwongozo maishani. Nyingi za methali hizo ziliandikwa na Sulemani

JE, Yehova ni Mtawala mwenye hekima? Njia moja yenye kuridhisha ya kujibu swali hilo ni kuchunguza mashauri anayotoa. Je, yanafanya kazi? Je, kuyatumia kunafanya maisha yawe mazuri zaidi na yenye kusudi? Mfalme Sulemani mwenye hekima aliandika mamia ya methali. Methali hizo zinazungumzia nyanja zote za maisha. Fikiria mifano kadhaa.

Kumtegemea Mungu. Ili kuwa na uhusiano mzuri pamoja na Yehova, lazima tumtegemee. Sulemani aliandika: “Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Mtambue yeye katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako.” (Methali 3:5, 6) Kumtegemea Mungu kwa kufuata mwongozo wake na kumtii hufanya maisha yawe na kusudi. Mtu anayefanya hivyo huufurahisha moyo wa Mungu na kumpa Yehova jibu la masuala yaliyozushwa na mpinzani Wake, Shetani.—Methali 27:11.

Kushughulika na watu wengine kwa hekima. Leo, kuliko wakati mwingine wowote, tunafaidika na shauri la Mungu kwa waume, wake, na watoto. “Ushangilie pamoja na mke wa ujana wako,” Mungu awashauri waume, akiwaagiza wawe waaminifu kwa wake zao. (Methali 5:18-20) Wanawake walioolewa wanaweza kufaidika na ufafanuzi wenye kupendeza ulio katika kitabu cha Methali kuhusu mke mwenye uwezo anayejipatia sifa kutoka kwa mumewe na watoto wake. (Methali, sura ya 31) Nao watoto wanaagizwa wawatii wazazi wao. (Methali 6:20) Kitabu hicho kinaonyesha kwamba urafiki ni muhimu, kwa kuwa kujitenga hutokeza ubinafsi. (Methali 18:1) Marafiki wanaweza kuwa na uvutano mzuri au mbaya, kwa hiyo tunapaswa kuwachagua kwa uangalifu.—Methali 13:20; 17:17.

Kujitunza kwa hekima. Kitabu cha Methali kina mashauri mazuri kuhusu kuepuka matumizi yasiyofaa ya vileo, kusitawisha hisia zinazofaa na kuondolea mbali zisizofaa, na kuwa mfanyakazi mwenye bidii. (Methali 6:6; 14:30; 20:1) Kitabu hicho kinaonya kwamba kutegemea akili ya mwanadamu na kupuuza shauri la Mungu hutokeza msiba. (Methali 14:12) Kinatuhimiza tumlinde yule mtu wa ndani, moyo wetu, dhidi ya uvutano mbalimbali usiofaa, na kutukumbusha kwamba katika moyo “ndiko zinakotoka chemchemi za uzima.”—Methali 4:23.

Mamilioni ya watu ulimwenguni wamejionea kwamba kuishi kupatana na mashauri hayo hufanya maisha yawe mazuri zaidi. Kwa sababu hiyo, wana sababu nzuri ya kumkubali Yehova kuwa Mtawala wao.

—Inatoka kwenye Kitabu cha Methali.

  • Tunaweza kujifunza nini kwa kuchunguza kitabu cha Methali?

  • Ni mwongozo gani ambao kitabu cha Methali kinatoa kuhusu kumtegemea Mungu na kushughulika kwa hekima na watu wengine, na pia tunapojitunza?

MHUBIRI

Mtu anaweza kupata maisha yenye kusudi na yenye kuridhisha jinsi gani? Kati ya watu wote, Sulemani hasa angeweza kupata jibu la swali hilo. Kwa kuwa alikuwa na utajiri mwingi, hekima, na mamlaka, angeweza kufanya uchunguzi na kuona ikiwa vitu hivyo vinaleta furaha ya kweli maishani. Aliishi maisha ya anasa, akaoa wanawake wengi warembo, na kufurahia burudani bora zaidi. Alianzisha miradi mikubwa ya ujenzi. Alichunguza maandishi ya wasomi. Alipata jibu gani? “Kila kitu ni ubatili.” Hata hivyo, alikata kauli hii: “Huu ndio mwisho wa mambo, kila jambo limekwisha sikiwa: Mwogope Mungu wa kweli na kushika amri zake. Kwa maana huo ndio wajibu wote wa mwanadamu.” —Mhubiri 12:8, 13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki