12 Ng’ombe hao wakaenda moja kwa moja kwenye barabara inayoelekea Beth-shemeshi.+ Walibaki kwenye barabara hiyo kuu, nao walikuwa wakilia walipokuwa wakienda; hawakugeuka kulia wala kushoto. Wakati huo wote, watawala wa Wafilisti walikuwa wakitembea nyuma yao hadi kwenye mpaka wa Beth-shemeshi.