22 Mara moja mwanamke huyo mwenye hekima akaenda kuzungumza na watu wote, nao wakamkata kichwa Sheba mwana wa Bikri na kukitupa kwa Yoabu. Basi Yoabu akapiga pembe, nao wakatawanyika kutoka kwenye jiji hilo, kila mmoja akarudi nyumbani kwake;+ naye Yoabu akarudi Yerusalemu kwa mfalme.