26 Nabii huyo aliyekuwa amemrudisha njiani aliposikia habari hizo, mara moja akasema: “Ni yule mtu wa Mungu wa kweli aliyeasi agizo la Yehova;+ kwa hiyo Yehova alimkabidhi kwa simba, amrarue na kumuua, kulingana na neno la Yehova alilokuwa amemwambia.”+