25 Ndiyo sababu hasira ya Yehova inawaka dhidi ya watu wake,
Naye ataunyoosha mkono wake dhidi yao na kuwapiga.+
Milima itatetemeka,
Na maiti zao zitakuwa kama takataka barabarani.+
Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,
Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.