-
Kumbukumbu la Torati 31:16, 17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Sasa Yehova akamwambia Musa hivi: “Tazama! Unakaribia kufa,* na watu hawa wataanza kufanya ukahaba wa kiroho pamoja na miungu ya kigeni inayowazunguka katika nchi wanayoenda.+ Wataniacha na kuvunja agano langu+ ambalo nimefanya pamoja nao.+ 17 Wakati huo hasira yangu itawaka dhidi yao,+ nami nitawaacha+ na kuuficha uso wangu wasiuone+ mpaka watakapoangamia. Kisha baada ya kupatwa na misiba na mateso mengi,+ watasema, ‘Je, hatujapatwa na misiba hii kwa sababu Mungu wetu hayuko miongoni mwetu?’+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Yehova Mungu wa mababu zao aliendelea kuwaonya kupitia wajumbe wake, aliwaonya tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake na makao yake. 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki wajumbe wa Mungu wa kweli,+ wakadharau maneno yake+ na kuwakejeli manabii wake,+ mpaka ghadhabu ya Yehova ilipokuja dhidi ya watu wake,+ hivi kwamba hawangeweza kuponywa.
-