17 “Nawe, mwana wa binadamu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Waambie ndege wa kila aina na wanyama wote wa mwituni, “Kusanyikeni pamoja na mje. Kusanyikeni kuzunguka dhabihu yangu ninayowatayarishia, dhabihu kubwa kwenye milima ya Israeli.+ Mtakula nyama na kunywa damu.+