Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumatatu, Oktoba 13

Yehova huona ndani ya moyo.—1 Sam. 16:7.

Ikiwa pindi fulani tunapambana na hisia za kujiona hatufai, tunapaswa kukumbuka kwamba Yehova mwenyewe anatuvuta kwake. (Yoh. 6:44) Anaona sifa nzuri tulizo nazo ambazo huenda sisi wenyewe hatuzioni na anaujua moyo wetu. (2 Nya. 6:30) Hivyo, tunaweza kumwamini anaposema sisi ni wenye thamani. (1 Yoh. 3:​19, 20) Kabla ya kujifunza kweli, baadhi yetu tulifanya mambo ambayo huenda bado yanafanya tujihisi tukiwa na hatia. (1 Pet. 4:3) Hata Wakristo waaminifu wanapambana na mwelekeo wa kutenda dhambi. Je, moyo wako unakuhukumu? Ikiwa ndivyo, unaweza kutiwa moyo kujua kwamba watumishi wengine waaminifu wa Yehova wamekabiliana na hisia hizo pia. Kwa mfano, mtume Paulo alijihisi vibaya alipofikiria kuhusu udhaifu wake. (Rom. 7:24) Paulo alikuwa ametubu dhambi zake na kubatizwa. Hata hivyo, alijirejelea kuwa “mdogo zaidi kati ya mitume” na mtenda dhambi “wa kwanza kabisa.”—1 Kor. 15:9; 1 Tim. 1:15. w24.03 27 ¶5-6

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumanne, Oktoba 14

Waliiacha nyumba ya Yehova.—2 Nya. 24:18.

Somo moja ambalo tunaweza kujifunza kutokana na uamuzi mbaya wa Mfalme Yehoashi ni kwamba tunahitaji kuchagua marafiki ambao watatuchochea kufanya mambo mazuri—marafiki ambao wanampenda Yehova na wanaotaka kumfurahisha. Hatuhitaji kuchagua tu marafiki wenye umri kama wetu. Kumbuka kwamba Yehoashi alikuwa na umri mdogo sana kuliko rafiki yake, Yehoyada. Jiulize hivi kuhusu marafiki unaochagua: ‘Je, wananisaidia kuimarisha imani yangu kwa Yehova? Je, wananitia moyo kuishi kulingana na viwango vya Mungu? Je, wanazungumza kumhusu Yehova na kweli zake zenye thamani? Je, wanaheshimu viwango vya Mungu? Je, wananiambia tu mambo ambayo ninapenda kusikia au je, wana ujasiri wa kunirekebisha ninapokosea?’ (Met. 27:​5, 6, 17) Kwa kweli, ikiwa rafiki zako hawampendi Yehova, huwahitaji. Lakini ikiwa una marafiki ambao wanampenda Yehova, shikamana nao—watakusaidia kufanya mambo yanayofaa!—Met. 13:20. w23.09 9-10 ¶6-7

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatano, Oktoba 15

Mimi ndiye Alfa na Omega.—Ufu. 1:8.

Herufi alfa ndiyo ya kwanza katika alfabeti ya Kigiriki, na herufi omega ndiyo ya mwisho. Kwa kusema kwamba yeye ndiye “Alfa na Omega,” Yehova anatusaidia kuelewa kwamba anapoanza kufanya jambo fulani, lazima alikamilishe kwa mafanikio. Baada ya kuwaumba Adamu na Hawa, Yehova alisema hivi: “Zaeni, muwe wengi, muijaze dunia na kuitiisha.” (Mwa. 1:28) Wakati huo ni kama Yehova alikuwa akisema “Alfa.” Alieleza waziwazi kusudi lake kwamba wakati utafika ambapo dunia itajaa wazao wa Adamu na Hawa walio wakamilifu na watiifu, ambao wataigeuza dunia kuwa paradiso. Wakati huo ujao, kusudi lake litakapotimia, ni kana kwamba atasema “Omega.” Baada ya kukamilisha uumbaji wa “mbingu na dunia na kila kitu kilichomo,” Yehova alitoa uhakikisho huu. Alitoa uhakikisho kwamba atatimiza kusudi lake kwa ajili ya wanadamu na dunia. Lingetimizwa kikamili mwishoni mwa ile siku ya saba.—Mwa. 2:​1-3. w23.11 5 ¶13-14

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki