Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
Tangazo
Lugha mpya inayopatikana: Betsileo
  • Leo

Jumapili, Novemba 9

Usiogope.—Dan. 10:19.

Tunahitaji kufanya nini ili tusitawishe ujasiri? Huenda wazazi wetu wakatuhimiza tuwe jasiri, lakini hatuwezi kurithi sifa hiyo kutoka kwao kana kwamba ni mali ya familia yetu. Kupata ujasiri ni kama kujifunza ustadi mpya. Njia moja ya kuboresha ustadi huo ni kwa kutazama kwa makini matendo ya mwalimu, kisha kuiga mfano wake. Vivyo hivyo, tunajifunza kuwa jasiri kwa kutazama kwa makini jinsi wengine wanavyoonyesha sifa hiyo, kisha kuiga mfano wao. Kama Danieli, tunahitaji kulifahamu vizuri Neno la Mungu. Tunapaswa kusitawisha uhusiano wa karibu pamoja na Yehova kwa kuzungumza naye kwa uhuru na mara nyingi. Na tunahitaji kumtumaini Yehova, na kusadiki kwamba sikuzote atatusaidia. Kisha imani yetu itakapojaribiwa, tutakuwa na ujasiri. Mara nyingi watu wanaoonyesha ujasiri huheshimiwa na wengine. Pia, huenda wakawasaidia watu wenye mioyo minyoofu wamjue Yehova. Bila shaka, tuna sababu nzuri za kusitawisha ujasiri. w23.08 2 ¶2; 4 ¶8-9

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Novemba 10

Hakikisheni mambo yote.—1 The. 5:21.

Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “hakikisheni” lilitumiwa kuhusiana na kupima uhalisi wa madini yenye thamani. Hivyo, tunahitaji kupima mambo tunayosikia au tunayosoma ili kuthibitisha ukweli wake. Jambo hilo litakuwa muhimu hata zaidi kwetu dhiki kuu inapokaribia. Badala ya kukubali kila jambo ambalo watu wanasema, tunatumia uwezo wetu wa kufikiri ili kulinganisha mambo tunayosoma au yale tunayosikia na mambo ambayo Biblia na tengenezo la Yehova linasema. Tukifanya hivyo, hatutadanganywa na propaganda yoyote ya roho waovu au njia nyingine ya ujanja. (Met. 14:15; 1 Tim. 4:1) Wakiwa kikundi, watumishi wa Mungu wataokoka dhiki kuu. Hata hivyo, tukiwa mtu mmoja-mmoja hatujui mambo tutakayokabili wakati ujao. (Yak. 4:14) Ingawa hivyo, iwe tutaokoka dhiki kuu tukiwa hai au tutakufa kabla ya wakati huo, Yehova atatuthawabisha kwa kutupa uzima wa milele ikiwa tutaendelea kuwa waaminifu. Acheni sisi sote tuendelee kukazia fikira tumaini letu zuri na kuendelea kuwa tayari kwa ajili ya siku ya Yehova! w23.06 13 ¶15-16

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumanne, Novemba 11

[Amewafunulia] watumishi wake . . . siri yake.—Amo. 3:7.

Hatujui jinsi baadhi ya unabii wa Biblia utakavyotimizwa. (Dan. 12:​8, 9) Lakini kwa kuwa hatujui kikamili jinsi unabii fulani utakavyotimizwa, hilo halimaanishi kwamba hautatimizwa. Bila shaka, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atatufunulia mambo tunayohitaji kujua kwa wakati unaofaa, kama alivyofanya zamani. Tangazo la “amani na usalama” litatolewa. (1 The. 5:3) Kisha serikali za kisiasa za ulimwengu zitashambulia dini za uwongo na kuziangamiza. (Ufu. 17:​16, 17) Kisha zitashambulia watu wa Mungu. (Eze. 38:​18, 19) Matukio hayo yataongoza moja kwa moja kwenye vita vya mwisho vya Har–​Magedoni. (Ufu. 16:​14, 16) Tunaweza kuwa na hakika kwamba matukio hayo yatatokea hivi karibuni. Kabla wakati huo haujafika, acheni tuendelee kuonyesha uthamini wetu kwa Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo kwa kukazia uangalifu unabii wa Biblia na kuwasaidia wengine wafanye hivyo pia. w23.08 13 ¶19-20

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki