Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
Tangazo
Lugha mpya inayopatikana: Mbum
  • Leo

Jumamosi, Julai 12

Walimuua [Yehoashi] . . . , lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme.—2 Nya. 24:25.

Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wa Yehoashi? Alikuwa kama mti wenye mizizi mifupi ambao ulitegemezwa na nguzo, nguzo hiyo ilipoondolewa, yaani, Yehoyada alipokufa, upepo wa uasi-imani ulivuma na kumwangusha Yehoashi. Hilo ni somo lenye nguvu kwamba hatupaswi kumwogopa Mungu kwa sababu tu ya kuchochewa na Wakristo wenzetu, kutia ndani watu wa familia yetu. Ili tuendelee kuwa wenye nguvu kiroho, ni lazima tuimarishe ujitoaji wetu kimungu na woga wetu kumwelekea Mungu kwa kujifunza kwa ukawaida, kutafakari, na kusali. (Yer. 17:​7, 8; Kol. 2:​6, 7) Yehova hadai mengi kutoka kwetu. Jambo ambalo anataka tufanye linatajwa kwenye andiko la Mhubiri 12:​13, linalosema: “Mwogope Mungu wa kweli na ushike amri zake, kwa maana huu ndio wajibu wote wa mwanadamu.” Ikiwa tutamwogopa Mungu, tutafaulu kukabiliana na majaribu ya wakati ujao na kusimama imara. Hakuna kitu chochote kitakachoharibu urafiki wetu pamoja na Yehova. w23.06 19 ¶17-19

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumapili, Julai 13

Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.—Ufu. 21:5.

Mstari wa 5 unaanza kwa kusema hivi: “Yule aliyeketi kwenye kiti cha ufalme akasema.” (Ufu. 21:5a) Maneno hayo ni ya pekee kwa sababu ni mojawapo ya sehemu tatu katika kitabu cha Ufunuo ambapo Yehova mwenyewe anazungumza. Kwa hiyo, uhakikisho huo unatolewa, si na malaika mwenye nguvu, au hata Yesu aliyefufuliwa, bali na Yehova mwenyewe! Jambo hilo linathibitisha kwamba tunaweza kutumaini maneno ya Yehova yanayofuata. Kwa nini? Kwa sababu Yehova ‘hawezi kusema uwongo.’ (Tito 1:2) Hivyo, maneno tunayosoma kwenye Ufunuo 21:​5, 6 hakika yatatimia. Tuchunguze neno “Tazama!” Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “tazama!” limetumiwa mara kwa mara katika kitabu cha Ufunuo. Ni maneno gani yanayofuata baada ya alama ya mshangao? Mungu anasema: “Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Ni kweli kwamba Yehova anazungumza kuhusu mabadiliko ya wakati ujao, lakini kwake, ahadi hiyo ni hakika na itatimia, hivi kwamba anayazungumzia mabadiliko hayo kana kwamba tayari yanatukia.—Isa. 46:10. w23.11 3-4 ¶7-8

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Julai 14

Akaenda nje akalia kwa uchungu.—Mt. 26:75.

Mtume Petro alipambana na udhaifu wake mbalimbali. Fikiria mifano michache. Yesu alipoeleza jinsi ambavyo angeteseka na kufa ili kutimiza unabii wa Biblia, Petro alimkemea. (Marko 8:​31-33) Petro na wale mitume wengine walibishana tena na tena kuhusu yule aliyekuwa mkuu zaidi kati yao. (Marko 9:​33, 34) Usiku wa mwisho kabla ya kifo cha Yesu, Petro alimshambulia mwanamume fulani na kumkata sikio. (Yoh. 18:10) Usiku huohuo Petro alilemewa na woga na mara tatu akakana kwamba hamjui Yesu, rafiki yake. (Marko 14:​66-72) Baada ya hapo Petro alilia kwa uchungu. Yesu hakumwacha mtume huyo aliyekuwa amevunjika moyo sana. Baada ya Yesu kufufuliwa, alimpa Petro fursa ya kuonyesha kwamba bado anampenda. Yesu alimwalika Petro awe mchungaji mnyenyekevu wa kondoo wake. (Yoh. 21:​15-17) Petro aliitikia kwa njia nzuri. Alikuwa huko Yerusalemu siku ya Pentekoste na alikuwa miongoni mwa Wakristo wa kwanza kutiwa mafuta kwa roho takatifu. w23.09 22 ¶6-7

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki