Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
Tangazo
Lugha mpya inayopatikana: Mbum
  • Leo

Ijumaa, Julai 11

Nitakutendea . . . kwa fadhili.—Mwa. 19:21.

Unyenyekevu na huruma ya Yehova humchochea kuwa mwenye usawaziko. Kwa mfano, Yehova alionyesha unyenyekevu kabla ya kuharibu watu waovu huko Sodoma. Kupitia malaika wake, Yehova alimwagiza Loti mwadilifu akimbilie kwenye eneo lenye milima. Loti aliogopa kwenda huko. Basi, akaomba kwamba yeye na familia yake waruhusiwe kukimbilia huko Soari, mji mdogo ambao ulipaswa kuharibiwa. Yehova angeweza kusisitiza kwamba Loti anapaswa kufuata kikamili maagizo yaliyotolewa. Badala yake, alikubali ombi la Loti, ingawa hilo lilimaanisha kwamba mji wa Soari haungeharibiwa. (Mwa. 19:​18-22) Karne nyingi baadaye, Yehova aliwaonyesha huruma wakaaji wa Ninawi. Alimtuma nabii Yona atangaze kuhusu uharibifu ambao ungelipata jiji hilo na wakaaji wake waovu. Lakini Waninawi walipotubu, Yehova aliwahurumia, naye hakuharibu jiji hilo.—Yona 3:​1, 10; 4:​10, 11. w23.07 21 ¶5

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumamosi, Julai 12

Walimuua [Yehoashi] . . . , lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme.—2 Nya. 24:25.

Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wa Yehoashi? Alikuwa kama mti wenye mizizi mifupi ambao ulitegemezwa na nguzo, nguzo hiyo ilipoondolewa, yaani, Yehoyada alipokufa, upepo wa uasi-imani ulivuma na kumwangusha Yehoashi. Hilo ni somo lenye nguvu kwamba hatupaswi kumwogopa Mungu kwa sababu tu ya kuchochewa na Wakristo wenzetu, kutia ndani watu wa familia yetu. Ili tuendelee kuwa wenye nguvu kiroho, ni lazima tuimarishe ujitoaji wetu kimungu na woga wetu kumwelekea Mungu kwa kujifunza kwa ukawaida, kutafakari, na kusali. (Yer. 17:​7, 8; Kol. 2:​6, 7) Yehova hadai mengi kutoka kwetu. Jambo ambalo anataka tufanye linatajwa kwenye andiko la Mhubiri 12:​13, linalosema: “Mwogope Mungu wa kweli na ushike amri zake, kwa maana huu ndio wajibu wote wa mwanadamu.” Ikiwa tutamwogopa Mungu, tutafaulu kukabiliana na majaribu ya wakati ujao na kusimama imara. Hakuna kitu chochote kitakachoharibu urafiki wetu pamoja na Yehova. w23.06 19 ¶17-19

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumapili, Julai 13

Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.—Ufu. 21:5.

Mstari wa 5 unaanza kwa kusema hivi: “Yule aliyeketi kwenye kiti cha ufalme akasema.” (Ufu. 21:5a) Maneno hayo ni ya pekee kwa sababu ni mojawapo ya sehemu tatu katika kitabu cha Ufunuo ambapo Yehova mwenyewe anazungumza. Kwa hiyo, uhakikisho huo unatolewa, si na malaika mwenye nguvu, au hata Yesu aliyefufuliwa, bali na Yehova mwenyewe! Jambo hilo linathibitisha kwamba tunaweza kutumaini maneno ya Yehova yanayofuata. Kwa nini? Kwa sababu Yehova ‘hawezi kusema uwongo.’ (Tito 1:2) Hivyo, maneno tunayosoma kwenye Ufunuo 21:​5, 6 hakika yatatimia. Tuchunguze neno “Tazama!” Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “tazama!” limetumiwa mara kwa mara katika kitabu cha Ufunuo. Ni maneno gani yanayofuata baada ya alama ya mshangao? Mungu anasema: “Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Ni kweli kwamba Yehova anazungumza kuhusu mabadiliko ya wakati ujao, lakini kwake, ahadi hiyo ni hakika na itatimia, hivi kwamba anayazungumzia mabadiliko hayo kana kwamba tayari yanatukia.—Isa. 46:10. w23.11 3-4 ¶7-8

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki