Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumatano, Julai 16

Yehova anajua kwamba kufikiri kwa watu wenye hekima ni ubatili.—1 Kor. 3:20.

Ni lazima tuepuke kutumia njia ya kufikiri ya wanadamu. Ikiwa tutaona mambo kulingana na maoni ya wanadamu, huenda tukampuuza Yehova na viwango vyake. (1 Kor. 3:19) Mara nyingi, “hekima ya ulimwengu huu” huchochea tamaa za mwili. Baadhi ya Wakristo huko Pergamamu na Thiatira waliwaiga watu waliowazunguka ambao walikuwa na maadili mapotovu na waliabudu sanamu. Yesu aliyapatia makutaniko hayo mawili shauri kali kwa sababu ya kuvumilia uasherati. (Ufu. 2:​14, 20) Leo, tunashawishiwa kukubali maoni yasiyofaa. Huenda watu wa familia yetu na marafiki wakajaribu kutusadikisha kwamba tuna msimamo mkali sana na kwamba hatupaswi kufuata sheria za Yehova. Kwa mfano, huenda wakadai kwamba si jambo muhimu kuendelea kuwa safi kiadili na viwango vya maadili vya Biblia vimepitwa na wakati. Nyakati nyingine, huenda tukafikiri kwamba mwongozo ambao Yehova anatupatia hautoshi. Hata huenda tukashawishiwa ‘kupita mambo yaliyoandikwa.’—1 Kor. 4:6. w23.07 16 ¶10-11

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Alhamisi, Julai 17

Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote naye ni ndugu ambaye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.—Met. 17:17.

Maria, mama ya Yesu, alihitaji kutiwa nguvu. Angekuwa mjamzito, ingawa hakuwa amefunga ndoa. Hakuwa na uzoefu wa kulea watoto wake mwenyewe, lakini angemtunza mvulana ambaye baadaye angekuwa Masihi. Na kwa kuwa hakuwa amefanya ngono, Maria angemwelezaje jambo hilo Yosefu, mchumba wake? (Luka 1:​26-33) Maria alipataje nguvu alizohitaji? Alitafuta msaada kutoka kwa watu wengine. Kwa mfano, alimwomba malaika Gabrieli ampe habari zaidi kuhusu mgawo huo. (Luka 1:34) Muda mfupi baada ya hapo, alisafiri kwenda kwenye “eneo lenye milima” la Yuda ili kumtembelea Elisabeti, mtu wake wa ukoo. Elisabeti alimpongeza Maria na aliongozwa na Yehova kusema unabii wenye kutia moyo kumhusu mwana wa Maria ambaye bado hakuwa amezaliwa. (Luka 1:​39-45) Maria alisema kwamba Yehova alikuwa “amefanya mambo makuu kwa mkono wake.” (Luka 1:​46-51) Kupitia malaika Gabrieli na Elisabeti, Yehova alimwimarisha Maria. w23.10 14-15 ¶10-12

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Ijumaa, Julai 18

Alitufanya tuwe ufalme, makuhani kwa Mungu na Baba yake.—Ufu. 1:6.

Idadi hususa ya wanafunzi wa Kristo wametiwa mafuta kwa roho takatifu, nao wana uhusiano wa pekee pamoja na Yehova. Wakristo hao 144,000 watatumikia wakiwa makuhani mbinguni pamoja na Yesu. (Ufu. 14:1) Patakatifu pa hema la ibada panafananisha hali yao ya kuzaliwa kwa roho na kuwa wana wa Mungu wakiwa bado duniani. (Rom. 8:​15-17) Patakatifu Zaidi pa hema la ibada panafananisha mbinguni, ambako Yehova anaishi. “Pazia” lililotenganisha Patakatifu na Patakatifu Zaidi lilifananisha mwili wa kibinadamu wa Yesu ambao ulikuwa kizuizi cha kuingia mbinguni akiwa Kuhani Mkuu sana wa hekalu la kiroho. Kwa kuutoa uhai wake wa kibinadamu uwe dhabihu kwa ajili ya wanadamu, Yesu alifungua njia ya uhai wa mbinguni kwa ajili ya Wakristo watiwa-mafuta. Ili wapokee thawabu yao ya mbinguni, ni lazima wao pia wavue miili yao ya kibinadamu.—Ebr. 10:​19, 20; 1 Kor. 15:50. w23.10 28 ¶13

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki