Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
Tangazo
Lugha mpya inayopatikana: Mbum
  • Leo

Jumapili, Julai 27

[Uweze] kutia moyo . . . na pia kuwakaripia.—Tito 1:9.

Ili uwe mwanamume Mkristo mkomavu, utahitaji kujifunza stadi zinazofaa. Stadi hizo zitakusaidia kutimiza majukumu yako kutanikoni, kupata kazi itakayokutegemeza wewe au familia yako, na zitakusaidia kuwa na uhusiano mzuri na wengine. Kwa mfano, jifunze kusoma na kuandika vizuri. Biblia inasema kwamba mwanamume mwenye furaha na mwenye mafanikio hutumia muda kila siku kusoma Neno la Mungu na kulitafakari. (Zab. 1:​1-3) Kwa kusoma Biblia kila siku, atajua njia ya Yehova ya kufikiri ambayo itamsaidia kufikiria mambo kwa njia nzuri, na kujifunza jinsi ya kutumia Maandiko vizuri. (Met. 1:​3, 4) Ndugu na dada zetu wanahitaji msaada wa wanaume wenye uwezo wa kufundisha na kuwapa ushauri unaotegemea Biblia. Ikiwa unajua kusoma na kuandika vizuri, utaweza kuandaa hotuba na maelezo yenye habari zenye kujenga na kuimarisha imani. Pia, utaweza kuandika mambo makuu kwa njia nzuri itakayokusaidia kujenga imani yako na kuwatia moyo wengine. w23.12 26-27 ¶9-11

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Julai 28

Yule aliye katika muungano na ninyi ni mkuu kuliko yule aliye katika muungano na ulimwengu.—1 Yoh. 4:4.

Unapoogopa, tafakari mambo ambayo Yehova atafanya wakati ujao Shetani atakapoondolewa. Onyesho lililotolewa kwenye programu ya kusanyiko la eneo la mwaka wa 2014 lilionyesha baba akizungumza na familia yake kuhusu jinsi ambavyo maneno ya 2 Timotheo 3:​1-5 yangesomwa ikiwa mistari hiyo iliyotabiriwa ingezungumzia hali zitakavyokuwa katika Paradiso. Alisema hivi: “Katika ulimwengu mpya, kutakuwa na nyakati zenye furaha sana. Maana watu watakuwa wenye kupendana, wenye kupenda mambo ya kiroho, wenye kiasi, wanyenyekevu, wenye kumsifu Mungu, wanaotii wazazi, wenye shukrani, washikamanifu, walio na upendo wa asili, wanaotaka makubaliano, wanaosema mema kuhusu wengine sikuzote, wanaojizuia, wapole, wanaopenda wema, wanaotumainika, wenye kutii, wanyenyekevu katika akili, wanaompenda Mungu badala ya kupenda raha, wakichochewa na upendo wa kweli kwa Mungu; nawe shikamana na watu hao.” Je, wewe huzungumza na watu wa familia yako au waabudu wenzako kuhusu jinsi maisha yatakavyokuwa katika ulimwengu mpya? w24.01 6 ¶13-14

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumanne, Julai 29

Nimekukubali.—Luka 3:22.

Tunafurahi sana kujua kwamba Yehova anawakubali watu wake wakiwa kikundi! Biblia inasema hivi: “Yehova anawafurahia watu wake.” (Zab. 149:4) Hata hivyo, wakati mwingine baadhi ya watu wanavunjika moyo na kujiuliza, ‘Je, Mungu ananikubali mimi binafsi?’ Watumishi wengi waaminifu wa Yehova walioishi nyakati za Biblia, pindi fulani walihangaishwa na mawazo kama hayo. (1 Sam. 1:​6-10; Ayu. 29:​2, 4; Zab. 51:11) Biblia inaonyesha wazi kwamba wanadamu wasio wakamilifu wanaweza kupata kibali cha Yehova. Jinsi gani? Ni lazima tuonyeshe kwamba tunamwamini Yesu Kristo na kubatizwa. (Yoh. 3:16) Hivyo, tunaonyesha hadharani kwamba tumetubu dhambi zetu na tumemwahidi Mungu kuwa tutafanya mapenzi yake. (Mdo. 2:38; 3:19) Yehova anafurahi tunapochukua hatua hizo ili kusitawisha uhusiano mzuri pamoja naye. Maadamu tunaendelea kufanya yote tuwezayo ili kuishi kulingana na ahadi tuliyotoa tulipojiweka wakfu, Yehova anatukubali na kutuona kuwa rafiki zake wa karibu.—Zab. 25:14. w24.03 26 ¶1-2

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki