Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumatatu, Julai 7

Mtumikieni Yehova kwa kushangilia. Njooni mbele zake kwa kelele za shangwe.—Zab. 100:2.

Yehova anataka tumtumikie kwa furaha na kwa hiari. (2 Kor. 9:7) Hivyo je, bado tunapaswa kufanyia kazi lengo la kiroho ikiwa hatuna tamaa ya kufanya hivyo? Fikiria mfano wa mtume Paulo. Alisema hivi: “Ninautia nidhamu sana mwili wangu na kuuongoza kama mtumwa.” (1 Kor. 9:​25-27, maelezo ya chini) Paulo alijilazimisha kufanya jambo lililofaa hata alipokosa tamaa ya kufanya hivyo. Je, Yehova alifurahishwa na utumishi wa Paulo? Bila shaka! Na Yehova alimbariki kwa sababu ya jitihada zake. (2 Tim. 4:​7, 8) Vivyo hivyo, Yehova anafurahi kuona tukifanyia kazi lengo letu hata ikiwa hatuna tamaa ya kufanya hivyo. Anafurahi kwa sababu ingawa hatufanyi kila mara jambo hilo kwa sababu tunalipenda, anajua kwamba tunalifanya kwa sababu tunampenda yeye. Kama vile Yehova alivyombariki Paulo, atabariki jitihada zetu pia. (Zab. 126:5) Na tunapoona baraka za Yehova, huenda tukachochewa zaidi. w23.05 29 ¶9-10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumanne, Julai 8

Siku ya Yehova inakuja.—1 The. 5:2.

Mtume Paulo aliwalinganisha wale ambao hawataokoka siku ya Yehova na watu wanaolala usingizi. Hawajui mambo yanayoendelea katika mazingira yanayowazunguka na pia hawajui muda. Hivyo, hawawezi kutambua matukio muhimu au kuchukua hatua inayofaa. Leo, watu wengi wamelala usingizi wa kiroho. (Rom. 11:8) Hawaamini mambo yanayothibitisha kwamba tunaishi katika “siku za mwisho” na kwamba dhiki kuu itakuja hivi karibuni. (2 Pet. 3:​3, 4) Hata hivyo, sisi tunatambua kwamba shauri lililoongozwa na roho la kuendelea kukaa macho linaendelea kuwa muhimu zaidi kadiri siku zinavyopita. (1 The. 5:6) Hivyo, ni lazima tuendelee kuwa watulivu na thabiti. Kwa nini? Ili tusianze kujihusisha na mambo ya kisiasa au ya kijamii katika ulimwengu huu. Mkazo wa kuunga mkono upande fulani kuhusiana na mambo hayo utazidi kuongezeka kadiri siku ya Yehova inavyokaribia. Ingawa hivyo, hatupaswi kuhangaika kuhusu jinsi tutakavyotenda. Roho ya Mungu inaweza kutusaidia kuwa na utulivu na kuwa thabiti kiakili na hivyo tufanye maamuzi kwa hekima.—Luka 12:​11, 12. w23.06 10 ¶6-7

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatano, Julai 9

Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, nikumbuke, tafadhali, na kunitia nguvu.—Amu. 16:28.

Unafikiria kuhusu nini unaposikia jina Samsoni? Inawezekana kwamba unamfikiria mwanamume aliyekuwa na nguvu sana. Hilo ni kweli. Lakini Samsoni alifanya uamuzi mbaya uliomsababishia mateso mengi. Hata hivyo, Yehova alikazia fikira mambo yote ambayo Samsoni alikuwa amefanya ili kumtumikia kwa uaminifu, na alitia ndani mfano wa Samsoni katika Biblia ili kutunufaisha. Yehova alimtumia Samsoni kutimiza mambo yenye kustaajabisha ili kuwasaidia watu aliowachagua, Waisraeli. Karne nyingi baada ya kifo cha Samsoni, Yehova alimwongoza mtume Paulo kutia ndani jina la Samsoni kwenye orodha ya wanaume waliokuwa na imani ya pekee. (Ebr. 11:​32-34) Mfano wa Samsoni unaweza kututia moyo. Alimtegemea Yehova, hata alipokabili hali ngumu. Tunaweza kutiwa moyo na pia kujifunza masomo fulani kutokana na mfano wake. w23.09 2 ¶1-2

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki