Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
Tangazo
Lugha mpya inayopatikana: Mbum
  • Leo

Jumanne, Julai 8

Siku ya Yehova inakuja.—1 The. 5:2.

Mtume Paulo aliwalinganisha wale ambao hawataokoka siku ya Yehova na watu wanaolala usingizi. Hawajui mambo yanayoendelea katika mazingira yanayowazunguka na pia hawajui muda. Hivyo, hawawezi kutambua matukio muhimu au kuchukua hatua inayofaa. Leo, watu wengi wamelala usingizi wa kiroho. (Rom. 11:8) Hawaamini mambo yanayothibitisha kwamba tunaishi katika “siku za mwisho” na kwamba dhiki kuu itakuja hivi karibuni. (2 Pet. 3:​3, 4) Hata hivyo, sisi tunatambua kwamba shauri lililoongozwa na roho la kuendelea kukaa macho linaendelea kuwa muhimu zaidi kadiri siku zinavyopita. (1 The. 5:6) Hivyo, ni lazima tuendelee kuwa watulivu na thabiti. Kwa nini? Ili tusianze kujihusisha na mambo ya kisiasa au ya kijamii katika ulimwengu huu. Mkazo wa kuunga mkono upande fulani kuhusiana na mambo hayo utazidi kuongezeka kadiri siku ya Yehova inavyokaribia. Ingawa hivyo, hatupaswi kuhangaika kuhusu jinsi tutakavyotenda. Roho ya Mungu inaweza kutusaidia kuwa na utulivu na kuwa thabiti kiakili na hivyo tufanye maamuzi kwa hekima.—Luka 12:​11, 12. w23.06 10 ¶6-7

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatano, Julai 9

Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, nikumbuke, tafadhali, na kunitia nguvu.—Amu. 16:28.

Unafikiria kuhusu nini unaposikia jina Samsoni? Inawezekana kwamba unamfikiria mwanamume aliyekuwa na nguvu sana. Hilo ni kweli. Lakini Samsoni alifanya uamuzi mbaya uliomsababishia mateso mengi. Hata hivyo, Yehova alikazia fikira mambo yote ambayo Samsoni alikuwa amefanya ili kumtumikia kwa uaminifu, na alitia ndani mfano wa Samsoni katika Biblia ili kutunufaisha. Yehova alimtumia Samsoni kutimiza mambo yenye kustaajabisha ili kuwasaidia watu aliowachagua, Waisraeli. Karne nyingi baada ya kifo cha Samsoni, Yehova alimwongoza mtume Paulo kutia ndani jina la Samsoni kwenye orodha ya wanaume waliokuwa na imani ya pekee. (Ebr. 11:​32-34) Mfano wa Samsoni unaweza kututia moyo. Alimtegemea Yehova, hata alipokabili hali ngumu. Tunaweza kutiwa moyo na pia kujifunza masomo fulani kutokana na mfano wake. w23.09 2 ¶1-2

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Alhamisi, Julai 10

Mjulisheni Mungu maombi yenu.—Flp. 4:6.

Tunaweza kusitawisha sifa ya uvumilivu kwa kuzungumza na Yehova kwa ukawaida kuhusu mambo yanayotuhangaisha. (1 The. 5:17) Labda sasa hukabiliani na jaribu kali. Hata hivyo, je, wewe hutafuta mwongozo wa Yehova kila mara unapokasirika, unapochanganyikiwa, au kulemewa na hisia? Ikiwa sasa unamwomba Mungu msaada kwa ukawaida unapokabiliana na changamoto za kila siku, hutasita kufanya hivyo utakapokabili changamoto kubwa zaidi wakati ujao. Utakuwa na uhakika kwamba Yehova anajua kihususa wakati na jinsi ya kukusaidia. (Zab. 27:​1, 3) Itakuwa rahisi zaidi kwetu kuvumilia dhiki kuu wakati ujao ikiwa sasa tunavumilia majaribu. (Rom. 5:3) Kwa nini tunasema hivyo? Ndugu wengi wametambua kwamba kila jaribu la imani walilovumilia liliwasaidia kuvumilia jaribu lililofuata. Uvumilivu uliwasaidia kuimarisha imani yao kwamba Yehova yuko tayari na anataka kuwasaidia. Kisha imani yao iliwasaidia kuvumilia jaribu lililofuata.—Yak. 1:​2-4. w23.07 3 ¶7-8

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki