Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa Bwana
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Katika 1912, Russell na washirika wake walijasiria kuanzisha jambo la kielimu lililokuwa la utaalamu ambao haukujulikana wakati huo. Kwa kweli, lingefikia mamilioni ya watu ulimwenguni pote. Ilikuwa ile “Photo-Drama of Creation” (Drama-Picha ya Uumbaji)—muunganisho wa picha ya sinema na utoaji wa slaidipicha, ukiambatanishwa na muziki uliorekodiwa na hotuba zilizorekodiwa katika rekodi za santuri. Ilikuwa yenye urefu wa saa zapata nane na ilitolewa katika sehemu nne. Licha ya “Photo-Drama” ya kawaida, ile “Eureka Drama,” iliyokuwa yenye mihadhara iliyorekodiwa na mirekodi ya muziki au rekodi pamoja na slaidi, ilifanywa ipatikane pia. Ingawa hiyo haikuwa na picha ya sinema, ilitolewa kwa mafanikio katika maeneo yasiyokuwa na idadi kubwa ya watu.

      Ebu wazia mandhari hiyo ya kihistoria: Katika Januari 1914, wakati wa enzi ya sinema zisizo na sauti,g wasikilizaji 5,000 walikusanyika katika The Temple, jengo moja kwenye West 63rd Street, katika New York City. Ilikuwa lazima kuzuia wengi zaidi wasiingie kwa kukosa nafasi. Ilikuwa pindi gani? Lo! wonyesho wa kwanza katika New York wa “Photo-Drama of Creation”! Mbele ya wasikilizaji kulikuwapo kiwambo kikubwa cha kuonyeshea picha ya sinema. Walipokuwa wakitazama—na kusikiliza—jambo fulani lenye kustaajabisha kwelikweli likatukia. C. T. Russell, wakati huo akiwa katika miaka yake ya mapema ya 60, akatokea katika kiwambo. Midomo yake ikaanza kusema, na maneno yake yangeweza kusikika! Utoaji ulipoendelea, ulipeleka wahudhuriaji—kwa njia ya maneno, picha za rangi, na muziki—kutoka uumbaji wa dunia mpaka mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo. Katika pindi ya utoaji waliona pia (kwa njia ya upigaji picha wa kuongeza mwendo) mambo mengine ambayo yalistaajabisha—kufunuka kwa ua na kuanguliwa kwa kifaranga. Walivutiwa kwelikweli!

      Kufikia mwisho wa 1914, “Photo-Drama” ilikuwa imetolewa kwa mamilioni ya watu katika Amerika Kaskazini, Ulaya, New Zealand, na Australia. Hakika “Photo-Drama” ilithibitika kuwa njia yenye mafanikio sana ya kufikia halaiki za watu katika kipindi kifupi cha wakati.

      Kwa wakati huohuo, namna gani juu ya Oktoba 1914? Kwa miongo ya miaka Russell na washirika wake walikuwa wamekuwa wakipiga mbiu kwamba Nyakati za Mataifa zingekoma katika 1914. Matarajio yalikuwa makubwa. C. T. Russell alikuwa amechambua wale waliokuwa wameweka tarehe mbalimbali za kurudi kwa Bwana, kama vile William Miller na baadhi ya vikundi vya Waadventisti wa Pili. Hata hivyo, tangu wakati wa ushirika wake wa mapema na Nelson Barbour, yeye alisadiki kwamba kulikuwa na kronolojia iliyokuwa sahihi, ikitegemea Biblia, na kwamba ilielekeza kwenye mwaka 1914 kuwa mwisho wa Nyakati za Mataifa.

      Mwaka huo wenye maana kubwa ulipokuwa ukikaribia, kulikuwa na matarajio makubwa miongoni mwa Wanafunzi wa Biblia, lakini yote waliyokuwa wakitarajia hayakuwa yamesemwa moja kwa moja katika Maandiko. Ni nini lingetukia?

  • Wakati wa Kutahini (1914-1918)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Sura ya 6

      Wakati wa Kutahini (1914-1918)

      “Acheni tukumbuke kwamba sisi tumo katika majira ya kutahini. . . . Ikiwa kuna sababu yoyote ambayo ingeongoza yeyote kuacha Bwana na Kweli Yake na kuacha kutoa dhabihu kwa ajili ya Kusudi la Bwana, basi si upendo wa Mungu tu ndani ya moyo ambao umesukuma kupendezwa katika Bwana, bali jambo jingine; labda kutumaini kwamba wakati ulikuwa mfupi; kujitakasa kulikuwa kwa wakati fulani tu. Ikiwa ndivyo, sasa ndio wakati ufaao wa kuacha.”

      MANENO hayo, yaliyotokea katika The Watch Tower la Novemba 1, 1914, yalifaa sana. Miaka ya kutoka 1914 hadi 1918, ilithibitika kwelikweli kuwa “majira ya kutahini” kwa Wanafunzi wa Biblia. Baadhi ya mitihani ilikuja kutoka ndani; mingine ilikuja kutoka nje. Ingawa hivyo, yote pamoja, ilitahini Wanafunzi wa Biblia katika njia ambayo ilifunua kama walikuwa kikweli na ‘upendo wa Mungu ndani ya mioyo yao.’ Je, wangeshikamana na “Bwana na Kweli Yake” au wangeacha?

      Matarajio Makubwa

      Katika Juni 28, 1914, Dyuki-Mkuu Francis Ferdinand wa Austria-Hungaria alipigwa risasi na kuuawa na mwuaji. Uuaji huo ulifyatusha ile Vita Kuu, kama vile Vita ya Ulimwengu 1 ilivyoitwa hapo kwanza. Vita ilianza katika Agosti 1914 wakati Ujerumani ilipovamia Ubelgiji na Ufaransa. Kufikia vuli ya mwaka huo, vita yenye umwagaji-damu mwingi sana ilikuwa imeanza.

      “Nyakati za Mataifa zimekwisha; siku za wafalme wao zimekwisha”! Ndivyo Ndugu Russell alivyopaaza sauti alipokuwa akiingia chumba cha kulia kwenye makao makuu ya Brooklyn ya Watch Tower Society, asubuhi ya Ijumaa, Oktoba 2, 1914. Msisimko ulikuwa mwingi. Wengi zaidi kati ya hao waliokuwapo walikuwa wametazamia kwa miaka mingi mwaka wa 1914. Lakini mwisho wa Nyakati za Mataifa ungeleta nini?

      Vita ya Ulimwengu 1 ilikuwa inachacha, na katika wakati huo ilikuwa imeaminiwa kwamba vita hiyo ilikuwa ikiongoza kuingia kwenye wakati wa machafuko ya utawala ya duniani pote ambayo yangetokeza mwisho wa mfumo wa mambo uliopo. Pia kulikuwa na matarajio mengine kuhusu mwaka 1914. Alexander H. Macmillan, ambaye alikuwa amebatizwa Septemba 1900, alikumbuka baadaye hivi: “Wachache kati yetu tulifikiri kwa uzito sana kwamba tungeenda mbinguni wakati wa juma la kwanza la mwezi huo wa Oktoba.”a Kwa kweli, akikumbuka asubuhi ambayo Russell alitangaza mwisho wa Nyakati za Mataifa, Macmillan alikubali hivi: “Tulisisimka sana sana, nami singeshangaa kama katika nukta hiyo tungeanza tu kupaa, huku tangazo la Russell likiwa ni ishara ya kuanza kupaa kuelekea mbinguni—lakini bila shaka hakukuwa na jambo lolote kama hilo.”

      Matarajio yaliyokatishwa tamaa kwa habari ya kurudi kwa Bwana Yesu katika karne ya 19 yalikuwa yamesababisha wafuasi wengi wa William Miller na vikundi vingine vya Waadventisti kupoteza imani. Lakini namna gani juu ya Wanafunzi wa Biblia walioshirikiana na Russell? Je, baadhi yao walikuwa wamevutwa na wazo la wokovu wao wenyewe wa mapema badala ya kumpenda Mungu na tamaa yenye nguvu ya kufanya mapenzi yake?

      ‘Ndugu Russell, Je, Wewe Hukukatishwa Tamaa?’

      Ndugu Russell alikuwa amekuwa akitia moyo Wanafunzi wa Biblia waendelee kukaa macho na kuazimia kuendelea katika kazi ya Bwana hata kama mambo hayatakamilika upesi kama wao walivyokuwa wametarajia.

      Oktoba 1914 ukapita, na C. T. Russell na washirika wake walikuwa wangali duniani. Kisha Oktoba 1915 ukapita. Je, Russell alikatishwa tamaa? Katika The Watch Tower la Februari 1, 1916, yeye aliandika hivi: “‘Lakini, Ndugu Russell, wazo lako ni nini kuhusu wakati wa kubadilika kwetu? Je, wewe hukukatishwa tamaa kwamba huo hukuja tulipoutazamia kwamba ungekuja?’ mtauliza. Hapana, twajibu, sisi hatukukatishwa tamaa. . . . Ndugu, wale miongoni mwetu walio na maoni yafaayo kuelekea Mungu hawakatishwi tamaa na mipango yoyote Yake. Sisi hatukutaka mapenzi yetu wenyewe yafanyike; hivyo wakati tulipopata kujua kwamba tulikuwa tukitarajia jambo lenye kosa katika Oktoba, 1914, basi tulifurahi kwamba Bwana hakubadili Mpango Wake utufae sisi. Sisi hatukutaka Yeye afanye hivyo. Sisi twataka tu tuweze kuelewa mipango na makusudi Yake.”

      Hapana, Wanafunzi wa Biblia ‘hawakuchukuliwa nyumbani’ mbinguni katika Oktoba 1914. Hata hivyo, Nyakati za Mataifa zilikwisha katika mwaka huo. Kwa wazi, Wanafunzi wa Biblia walikuwa na mengi ya kujifunza kuhusu umaana wa mwaka 1914. Kwa wakati huohuo, wafanye nini? Wafanye kazi! Kama vile The Watch Tower la Septemba 1, 1916, lilivyoeleza jambo hilo: “Sisi tuliwazia kwamba kazi ya Mavuno ya kukusanya kuleta ndani Kanisa [la watiwa-mafuta] ingekamilishwa kabla ya mwisho wa Nyakati za Mataifa; lakini hamkuwa na lolote katika Biblia lililosema hivyo. . . . Je, sisi twasikitika kwa sababu kazi ya Mavuno yaendelea? Hapana, hakika . . . Maoni yetu ya sasa, ndugu wapendwa, yapasa kuwa ya shukrani nyingi kuelekea Mungu, uthamini wenye kuongezeka wa Kweli nzuri ajabu ambayo Yeye ametujalia pendeleo la kuiona na kuhusianishwa nayo, na bidii yenye kuongezeka katika kupeleka Kweli hiyo kwa wengine waijue.”

      Lakini je, kulikuwa mengi zaidi ya kufanywa katika kazi ya mavuno? Kwa wazi Ndugu Russell alifikiri hivyo. Yenye kuonyesha hivyo ni mazungumzo aliyokuwa nayo pamoja na Ndugu Macmillan katika vuli ya 1916. Akimwita Macmillan kwenye ofisi yake alimofanyia funzo na uandishi wake kwenye Betheli ya Brooklyn, Russell alimwambia hivi: “Kazi inaongezeka haraka, na itaendelea kuongezeka, kwa kuwa kuna kazi ya ulimwenguni pote ya kufanywa katika kuhubiri ‘gospeli ya ufalme’ katika ulimwengu wote.” Russell alitumia muda wa saa tatu na nusu akieleza Macmillan kwa ufupi yale aliyoelewa kutoka Biblia kuwa ndiyo kazi kubwa iliyokuwa ingali mbele.

      Wanafunzi wa Biblia walikuwa wamepitia mtihani mgumu. Lakini kwa msaada wa The Watch Tower walikuwa wametiwa nguvu washinde kukatishwa tamaa. Hata hivyo, majira ya kutahini yalikuwa hayajakwisha.

      “Itakuwaje Sasa?”

      Katika Oktoba 16, 1916, Ndugu Russell na mwandishi wake Menta Sturgeon waliondoka kwenda katika safari ya kutoa mihadhara iliyokuwa imetangulia kupangiwa sehemu ya magharibi na kusini-magharibi mwa Marekani. Ingawa hivyo, Russell alikuwa mgonjwa mahututi wakati ule. Safari hiyo iliwapeleka kwanza Detroit, Michigan, kupitia Kanada. Kisha, baada ya kutua katika Illinois, Kansas, na Texas, wanaume hao wawili wakawasili California, ambako Russell alitoa hotuba yake ya mwisho siku ya Jumapili, Oktoba 29, huko Los Angeles. Siku mbili baadaye, mapema alasiri ya Jumanne, Oktoba 31, Charles Taze Russell mwenye umri wa miaka 64 alikufa akiwa ndani ya garimoshi katika Pampa, Texas. Tangazo la kifo chake lilitokea katika The Watch Tower la Novemba 15, 1916.

      Tokeo lilikuwa nini juu ya familia ya Betheli wakati habari za kifo cha Ndugu Russell zilipotangazwa? A. H. Macmillan, aliyetumika akiwa msaidizi wa Russell ofisini wakati Russell alipokuwa hayupo, alikumbuka baadaye asubuhi ile aliposomea familia ya Betheli barua ya simu: “Mguno ulisikika katika chumba hicho chote cha kulia. Baadhi yao walilia kwa sauti. Hakuna aliyekula kiamshakinywa asubuhi hiyo. Wote walikuwa wamehuzunika sana. Kwenye mwisho wa kipindi cha chakula walikutana vikundi vidogovidogo kuongea na kunong’onezeana, ‘Itakuwaje sasa?’ Ni kazi ndogo iliyofanywa siku hiyo. Sisi hatukujua la kufanya. Jambo hilo lilikuwa lisilotazamiwa kabisa, na hali Russell alikuwa amejaribu kututayarisha kwa ajili yalo. Tungefanya nini? Mshtuko wa kwanza wa hasara yetu ya kumpoteza C. T. Russell katika kifo ulikuwa ndio mbaya zaidi. Wakati ujao wetu ulikuwa wenye shaka sana katika siku hizo chache za kwanza. Muda wote wa maisha yake Russell alikuwa amekuwa ndiye ‘Sosaiti.’ Kazi ilitegemea azimio lake lenye nguvu la kuona mapenzi ya Mungu yakifanywa.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki